Nyaraka za Waislamu, Wakristo zamtisha JK
RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa nyaraka na kauli kali kali
zinazotolewa na viongozi wa dini za Kikristo na Kiislamu zimelifikisha
taifa mahali ambapo kama viongozi na waumini wa dini hizi hawatakubali
kubadili muelekeo wa sasa, nchi inakoelekea ni kubaya.
Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi kwa wananchi, Rais alisema licha
ya kulizungumzia suala hilo mara kadhaa lakini kutokana na nyaraka na
kauli hizo anashawishika kusema tena.
“Nyaraka na kauli hizo zina mambo mawili makuu. Kwanza, kwamba kila
upande unatuhumu, kushutumu na kulaumu upande mwingine kwa kufanya
vitendo viovu dhidi ya dini yake,” alisema.
Alisema kuwa kauli na mihadhara ya kudhalilisha dini za wengine,
kunajisi vitabu vitakatifu, kuchoma moto nyumba za ibada, mzozo kuhusu
nani achinje na kuuawa kwa viongozi wa dini ni baadhi ya mambo
yanayotolewa mifano.
“Jambo la tatu ninalopenda kuzungumza nanyi leo ni uhusiano wa
Waislamu na Wakristo nchini. Jambo hili nimeshalizungumzia mara kadhaa
siku za nyuma, lakini nalazimika kulisemea tena kutokana na hali ilivyo
sasa,” aliongeza.
Alisema Tanzania itaacha kuwa kisiwa cha amani na kuingia katika
orodha ya nchi zenye migogoro na hata vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Aidha Wakristo wanateswa na viongozi wao kuuawa na Waislamu, lakini
serikali haichukui hatua. Kwa ajili hiyo wanadai kuwa serikali
imeshindwa kulinda uhai wa raia wake. Wanasema pia kwamba serikali
inapendelea upande wa Waislamu.
“Waislamu nao wanadai kuwa kitabu chao kitakatifu, yaani Quran Tukufu,
kinadhalilishwa kwa kuchanwa, kuchomwa moto na kukojolewa na Wakristo
na serikali haichukui hatua yoyote ya maana,” alisema.
Alisema kuwa yeye binafsi anashutumiwa kuwa anapendelea kushiriki
zaidi kwenye shughuli za Wakristo kuliko za Waislamu kama vile harambee
za kujenga makanisa na shule za makanisa.
“Naambiwa kuwa mwepesi kushiriki maziko ya maaskofu kuliko masheikh
wanapofariki. Ipo misikiti mitatu hapa Dar es Salaam wamenisomea itikafu
nife. Katika itikafu hiyo wamewajumuisha Inspekta Jenerali wa Polisi,
Saidi Mwema, na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam,
Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Ndugu Suleiman Kova.
Post a Comment