ad

ad

Vijana washauriwa kuwa wabunifu

VIJANA nchini wametakiwa kuhakikisha wanatumia muda wao kufanya kazi na kubuni miradi mbalimbali badala ya kukaa vijijini wakisubiria ajira au wafadhili.

Wito huo ulitolewa na mkurugenzi wa kampuni ya Remapt’s Busness Co.Ldt, William Mligo, alipozungumza na waimbaji wa nyimbo za Injili pamoja na nyimbo za kijamii mjini hapa.
Mligo alisema vijana wengi wamekuwa na tabia ya kukaa vijiweni wakiomba misaada au kuendelea kulaumu badala ya kutumia muda wao kubuni miradi, ili kujikwamua na umaskini.

“Vijana wenzangu huwezi kuondokana na umaskini kama hutakuwa mbunifu. Ni lazima ufanye kazi na ukisha kuwa na pa kuanzia ndipo sasa unapoweza kutafuta wafadhili au kujiunga katika kikundi na kuwasilisha andiko kwa taasisi mbalimbali, ili kuomba msaada wa ufadhili,” alisema Mligo.

Aidha alisema licha ya kampuni yake kuwa inahusika na utangazaji kwa bidhaa mbalimbali, lakini pia inajihusisha na uibuaji wa vipaji kwa vijana na watoto hususan wa vijiji kwa lengo la kuwajengea uwezo na kutambua kuwa vipaji vingi vinaweza kutumiwa kama ajira.

Powered by Blogger.