TEMESA Yatangaza Nafasi 6 za Meneja wa Kanda, Maombi Mwisho Februari 20

Kwa niaba ya Wakala wa Huduma za Ufundi za Umeme, Mitambo na Elektroniki Tanzania (TEMESA), Ofisi ya Rais – Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (PSRS) inakaribisha maombi kutoka kwa Watanzania wenye sifa, weledi, uadilifu na ari ya kufanya kazi kujaza nafasi sita (6) za kazi kama ifuatavyo:
1. Nafasi: Meneja wa Kanda (Regional Manager) – Nafasi 6
Majukumu ya Kazi
Kusimamia uendeshaji wa shughuli za kanda kwa ufanisi na kuhakikisha huduma zinatolewa kwa wakati na kwa viwango vya ubora.
Kusimamia rasilimali za kazi zikiwemo vifaa, zana na mitambo bila kuzalisha gharama zisizo za lazima.
Kuboresha huduma kwa wateja kwa kuhakikisha malalamiko yanashughulikiwa haraka.
Kuongoza na kusimamia wasimamizi pamoja na wafanyakazi wa utawala.
Kuandaa na kusimamia bajeti ya kanda kwa kuzingatia matumizi yenye tija.
Kuratibu mafunzo kwa watumishi wa kiufundi ili kuongeza ujuzi.
Kushirikiana na timu za kiufundi kuboresha utoaji huduma.
Kutafuta fursa za kibiashara na kupanua wigo wa huduma za TEMESA ndani ya kanda husika.
Kujenga mahusiano mazuri na wadau, jamii na mamlaka za eneo.
Kuandaa taarifa za utendaji wa kanda mara kwa mara.
Kutekeleza majukumu mengine atakayopangiwa na msimamizi wake.
Sifa za Mwombaji
Mwombaji anatakiwa kuwa na:
Shahada ya Uzamili na Shahada ya Kwanza katika mojawapo ya fani zifuatazo:
Biashara (Fedha/Marketing), Fedha, Uchumi, Takwimu, Utawala wa Umma, au Uhandisi (Umeme, Mitambo, Elektroniki, Electromechanical).
Waombaji wa Uhandisi lazima wawe wamesajiliwa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) kama Professional Engineer.
Uzoefu wa kazi usiopungua miaka 8 katika fani husika.
Shahada ya Uzamili inayohusiana na Shahada ya Kwanza ni faida zaidi.
Mshahara
TMSS 10
Masharti ya Jumla
Mwombaji awe raia wa Tanzania na asiwe na umri zaidi ya miaka 45.
Aambatanishe nakala zilizothibitishwa za vyeti vyote muhimu (elimu, taaluma, cheti cha kuzaliwa n.k).
Wasitumie result slips, testimonials au partial transcripts.
Aweke picha ya passport size ya hivi karibuni.
Waajiriwa wa Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba.
Aonyeshe majina ya wadhamini (referees) watatu.
Vyeti vya nje ya nchi vihalalishwe na TCU/NECTA/NACTVET.
Jinsi ya Kutuma Maombi
Maombi yote yawasilishwe kupitia Recruitment Portal ya PSRS pekee.
Mwisho wa Kutuma Maombi: 20 Februari, 2026
Katibu,
Ofisi ya Rais,
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma,
S.L.P 2320, Dodoma.
Post a Comment