ad

ad

Je uwezo wa hospitali ya Taifa Muhimbili umeshuka?

Muhimbili ni hospitali ya rufaa ya taifa la Tanzania. Hospitali ambayo inatoa huduma ya juu katika katika sekta ya afya. Lakini siku za karibuni kumekuwepo na mijadala katika mitandao mbalimbali ya kijamii juu ya uwezo wa hospitali hii ya taifa. Mijadala hii iliibuka baada ya mkurengezi wa bmakosa ya jinai bwana Robert Manumba kuamia hospitali ya Aga Khan toka Muhimbili alipokuwa anatibiwa awali. Watu walihoji iwapo Muhimbili inatowa rufaa kwenda Aga khan. Jibu ni hapana.


Kiwango cha taaluma walichonacho madaktari wa Muhimbili ni kikubwa. Tena wengine ni wasomi waliobobea na maprofesa. Hivyo si kweli kwamba uwezo wa muhimbili umeshuka.

Ikumbukwe kuwa mgonjwa ana haki au matakwa ya kutibiwa hospitali yoyote nyingine  anayotaka. Hii inategemea mfumo wa jamii ulipo. Sekta ya afya haina tofauti na sekta nyingine  mfano elimu na ajira katika nchi yetu.

Mojawapo ya madai ya madktari katika migomo iliyopita ni kuboresha huduma za afya na kupunguza rufaa zisizokuwa na umuhimu nje ya nchi. Hii itasaidia kuokoa maisha ya watanzania wengi wasiokuwa na uwezo na hata kupunguza gharama kutoka kwa wafadhili na serikali ya kupeleka wagonjwa nje na kuwekeza katika sekta nyingine. Ni ajabu kama utampa mgonjwa mwenye malaria rufaa kwenda india kutibiwa. Je utatoa rufaa ngapi kwa mwaka?

Nani asiyefahamu hali ya hospitali zetu nchi. Hospitali nyingi zinawataalamu wachache na hazina vitendea kazi vya kutosha. Hospitali na vituo vya afya nchini viko katika hali mbaya. Hivyo watanzania wengi wanapoteza maisha hata kwa magonjwa ambayo yako katika uwezo wa wataalam.

Madaktari katika hospitali ya Taifa na hospitali nyingine wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu. Wengine wamekuwa hawautumii utaalamu wao ipasavyo. Hii imepelekea wengine kwenda nje ya nchi ambako watatumia ujuzi wao kwa malipo stahiki. Tanzania ni nchi ambayo wataalamu wake hawathaminiwi. Hivyo si kweli kwamba uwezo wa hospitali yetu ya taifa umeshuka.

Ni wajibu wa serikali kuhakikisha inaboresha mfumo wa afya. Lazima kuingoza  vitendea kazi na kuboresha maslahi ya wafanyabkazi wake. 
     Chanzo cha habari na www.paulmasua.com
Powered by Blogger.