38 wafariki dunia katika mafuriko nchini Msumbiji
Umoja wa Mataifa umesema kuwa mafuriko yaliyoiathiri Msumbiji yameua
watu 38 na kupelekea wengine 150,000 kukosa makazi.
Marie Conselee
Mukangendo Afisa wa Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF ameyasema
hayo katika mji wa Chokwe umbali wa kilomita 230 kaskazini mwa Maputo
mji mkuu wa Msumbiji.
Mukangendo amesema dola zisizopungua milioni 15
zinahitajika ili kuwahudumia waathirika wa mafuriko. Ameongeza kuwa hali
ya mambo ni mbaya katika kambi zinazowahifadhi watu waliopoteza makazi
yao kutokana na kukosekana huduma muhimu za msingi kama vyoo.
Itakumbukwa kuwa watu zaidi ya 700 walipoteza maisha kufuatia mafuriko
yaliyoikumba Msumbiji mwaka 2000.

Post a Comment