Lucy Komba: Mwacheni Irene Uwoya Alie...Hata Kama Wametengana
MKONGWE wa filamu nchini anayeishi Denmark, Lucy Komba amemtetea
msanii mwenzake Irene Uwoya aliyefiwa na aliyekuwa mumewe, Hamad
Ndikumana ‘Katauti’ na kuwataka watu kumuacha alie.
Akizungumza na Motomoto News, Lucy alisema watu wanaomponda Uwoya kuhusiana na kifo cha Ndikumana wanakosea kwani hakuna mtu ambaye amewahi kufiwa na mume au aliyekuwa mzazi mwenzake na asilie.
“Kiukweli Uwoya mwacheni alie tu hata kama walikuwa wametengana, lakini unaposikia mtu ambaye aliwahi kuwa mume, mpenzi au baba watoto wako amefariki lazima uumie, tena sana kwani kifo ni kitu kingine kabisa, wanaomshambulia wamwache maana wanamuonea tu,” alisema Lucy.
Akizungumza na Motomoto News, Lucy alisema watu wanaomponda Uwoya kuhusiana na kifo cha Ndikumana wanakosea kwani hakuna mtu ambaye amewahi kufiwa na mume au aliyekuwa mzazi mwenzake na asilie.
“Kiukweli Uwoya mwacheni alie tu hata kama walikuwa wametengana, lakini unaposikia mtu ambaye aliwahi kuwa mume, mpenzi au baba watoto wako amefariki lazima uumie, tena sana kwani kifo ni kitu kingine kabisa, wanaomshambulia wamwache maana wanamuonea tu,” alisema Lucy.
Post a Comment