Davina Atetea Viben’ten kwani mapenzi hayana umri
LICHA ya wengi kuwaponda wanawake wenye umri mkubwa wanaokuwa na
uhusiano wa kimapenzi na wanaume wadogo kiumri ‘viben’ten’, staa wa
filamu za Kibongo, Halima Yahya ‘Davina’ amewatetea kwa kusema siyo
vibaya kwani mapenzi hayana umri.
Akipiga stori na Za Motomoto News, Davina alisema licha ya kutowahi kuwa na kiben’ten, haoni tatizo kwa wanaokuwa na uhusiano na wanaume hao wadogo kwa kuwa siku zote mapenzi hayachagui umri, dini wala kabila bali mtu hujikuta amependa tu.
“Sijawahi kuwa na kiben’ten huwa naona ni bora kuwa na mtu ambaye tunalingana kiumri au amenizidi kidogo, wanawake wanaokuwa na wanaume hao wadogo siwezi kuwalaumu au kuwacheka kwa sababu mapenzi ni kitu ambacho hakizuiliki wala hakichagui,” alisema Davina.
Akipiga stori na Za Motomoto News, Davina alisema licha ya kutowahi kuwa na kiben’ten, haoni tatizo kwa wanaokuwa na uhusiano na wanaume hao wadogo kwa kuwa siku zote mapenzi hayachagui umri, dini wala kabila bali mtu hujikuta amependa tu.
“Sijawahi kuwa na kiben’ten huwa naona ni bora kuwa na mtu ambaye tunalingana kiumri au amenizidi kidogo, wanawake wanaokuwa na wanaume hao wadogo siwezi kuwalaumu au kuwacheka kwa sababu mapenzi ni kitu ambacho hakizuiliki wala hakichagui,” alisema Davina.
Post a Comment