ad

ad

SAMWEL SITTA MGOMBEA PEKEE UENYEKITI BUNGE LA KATIBA, CHENGE "ABWAGA MANYANGA"


Samwel Sitta.

Hatimaye mzee wa "Standards and Speed", Mbunge wa Urambo Mashariki (CCM), Samwel Sitta, ambaye pia ni Waziri wa Ushirikianmo wa Afrtika Mashariki, amepitishwa na chama chake, kuwa mgombea pekee wa nafasi ya Uenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba.


Taarifa kutoka Dodoma zilizonukuliwa na vyombo vya habari mapema Jumanne Asubuhi Machi 4, 2014, Samwel Sitta, spika mstaafu anayeelezwa kuleta mabadiliko makubwa ndani ya bunge la Muungano la vyama vingi, atasaidiwa na Samia Suluhu Hassan, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia masuala ya Muungano.

Taarifa hiyo ilisema, hatua ya Samwel Sitta kuteuliwa kuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo, inafuatia vikao virefu vya wabunge wa CCM vya kimkakati, ambapo aliyekuwa akitajwa kuwania nafasi hiyo, sambamba na Sitta, Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge alitangaza kujitoa.

Sitta sasa atapambana na wagombea kutoka upande wa upinzani, na haitarajiwi kushindwa.

Umaarufu wake, ulitokana na falsafa yake ya “Standard and Speed” ambapo, alitoa fursa karibu sawa kwa wabunge wote kutoka upinzani na chama chake, wakati wa kuchangia mijadala mbalimbali hata ile iliyoonekana kukibomoa chama chake.
Kuteuliwa kwake, kunatarajiwa kulichangamsha bunge  hilo maalum la Katiba ambalo wachambuzi wa mambo wanabashiri kuwa litakuwa gumu mmno kuliongoza, kwani kuna wajumbe wake, wanatoka kada mbalimbali na hivyo kulifanya kuwa ni bunge litakalohitaji busara na uvumilivu kuliongoza.
Powered by Blogger.