Hemedy na Najma kunani? Picha zao za kimahaba zavuja, ziko hapa
Waigizaji wa filamu nchini ambao pia ni wanamuziki wa Bongofleva
Hemedy Suleiman na Najma Datan wamezua maswali kwa watu wanaofuatilia
habari za mastaa wa Tanzania baada ya picha zao wakiwa kimahaba zaidi
kuanza kusambaa. Katika picha hizo zinazoonekana hapo chini wawili hao
wanabusiana kimahaba kama wapenzi walioshibana. Haijajulikana kama picha
hizo ni za video mpya ya muziki, filamu au ni wapenzi kweli.
Hata hivyo tayari inajulikana kuwa Hemedy kwasasa anatoka na Zuhura Gora
ambaye ni model na muigizaji pia, huku Najma akiwa ameshawahi kuwa
katika penzi na Mr.Blue kabla ya kuhisiwa kutoka kimapenzi na msanii
mwingine Diamond Platnumz.
-Habari kwa hisani ya SwahiliWorldPlanet-

Post a Comment