SUNZU AFUKUZWA MAZOEZINI SIMBA, AJIUNGA BONGO MUVI.
(Picha na Musa Mateja /GPL)
Na Wilbert Molandi
KOCHA Mkuu wa Simba, Patrick Liewig, juzi alimtimua straika wake wa kimataifa, Felix Sunzu katika mazoezi yake yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.
KOCHA Mkuu wa Simba, Patrick Liewig, juzi alimtimua straika wake wa kimataifa, Felix Sunzu katika mazoezi yake yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo la kushangaza liliwaacha midomo wazi baadhi ya
mashabiki wachache waliojitokeza uwanjani hapo, ambapo baada ya
kufukuzwa, Sunzu alisogea kwenye uwanja wa pembeni na kujiunga katika
mazoezi ya wachezaji wa Bongo Muvi yaliyokuwa yakiendelea muda huo.
Tukio
hilo limetokea ikiwa ni muendelezo wa adhabu ya baadhi ya wachezaji
wakongwe klabuni hapo kusimamishwa, chanzo kikiwa ni utovu wa nidhamu,
baadhi yao ni Haruna Moshi ‘Boban’, Komambil Keita, Mwinyi Kazimoto,
Ramadhani Chombo ‘Redondo’ na Amir Maftah.
Sunzu alifika mazoezini
hapo akiwa na jezi za timu hiyo kwa ajili ya kuungana na wenzake, lakini
dakika chache baadaye, mshambuliaji huyo aliitwa na Liewig na kutakiwa
kuondoka kwenye mazoezi yaliyosimamiwa na msaidizi wake (Liewig) Jamhuri
Kihwelo ‘Julio’ na Meneja, Moses Basena.
Sunzu akifuata programu ya mazoezi ya wachezaji hao wa
Bongo Muvi kwa umakini ikiwemo kukimbia mbio fupi na ndefu.
Taarifa za ndani zilieleza kuwa Kamati ya Utendaji ya timu hiyo ndiyo ilimruhusu Sunzu ajiunge na wenzake lakini kocha hakupewa taarifa.
Taarifa za ndani zilieleza kuwa Kamati ya Utendaji ya timu hiyo ndiyo ilimruhusu Sunzu ajiunge na wenzake lakini kocha hakupewa taarifa.
“Kilichotokea
katika mazoezi hayo, ni matatizo ya mawasiliano kati ya Kamati ya
Utendaji na kocha ambayo yalichelewa kumfikia kabla ya kumfukuza
mazoezini Sunzu,” kilisema chanzo.
Wakati huohuo, wakati tukienda mitamboni ilielezwa kuwa, Sunzu, Abdallah Juma na Kazimoto wanaweza kusamehewa, ambapo wametakiwa kuandika barua za kujieleza kisha warejeshwe kwa ajili ya mechi ya Yanga.
Wakati huohuo, wakati tukienda mitamboni ilielezwa kuwa, Sunzu, Abdallah Juma na Kazimoto wanaweza kusamehewa, ambapo wametakiwa kuandika barua za kujieleza kisha warejeshwe kwa ajili ya mechi ya Yanga.
Post a Comment