Tanzania yamtaka Rais wa Malawi aache kutapatapa.
Serikali ya Tanzania imeitaka Malawi iache kutoa maneno yasiyo na msingi
kuhusiana na mgogoro wa mipaka wa Ziwa Nyasa. Kauli hiyo rasmi ya
serikali ya Tanzania imetolewa na
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe
Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo,
Bernard Membe na imekuja baada ya Rais Joyce Banda wa Malawi kutangaza
katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa atapeleka suala hilo kwenye
Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ).
Membe amesema, Malawi inatakiwa
isubiri uamuzi wa jopo la usuluhishi lifanye kazi na litoe maamuzi yake.
Aidha serikali ya Tanzania imekanusha madai kupelekewa nyaraka za siri
kutoka kwa katibu wa jopo hilo na kusema madai hayo hayana msingi.
Kabla
ya hapo Rais wa Malawi alikuwa ameituhumu Tanzania kuwa, kuna Mtanzania
anayeitwa John Tesha ametoa habari za siri na kuiba nyaraka za siri
kutoka katika jopo hilo na kuikabidhi serikali ya Tanzania. Akilitolea
ufafanuzi jambo hili, Waziri Membe amesema kuwa, Tanzania na jopo hilo
limestushwa na madai hayo ya Rais wa Malawi. Membe aidha amewaambia
waandishi wa habari kuwa serikali ya Malawi inapaswa iache kutapatapa
mara Uingereza, mara Marekani, mara kwa Jumuia ya Madola na mara kwa
Umoja wa Afrika (AU) na kuonana viongozi mbalimbali wa dunia, bali
iamini kuwa jopo la Mzee Chissano linaweza kutatua tatizo hilo.

Post a Comment