Jaydee kuadhimisha miaka 10 katika fani.
MSANII nguli asiyechuja katika nyimbo zake, Judith Wambura,
‘Lady Jaydee’ amewashukuru wadau na mashabiki wake kwa kuendelea
kumuunga mkono na kumpa nguvu.
Akizungumzia sherehe za kutimiza miaka 13 tangu aanze kazi ya
muziki, Jaydee alisema kuwa ameandaa sherehe kabambe itakayoambatana na
uzinduzi wa albamu yake ya sita ‘Nothing But The Truth’.
“Kwa mwaka huu wa 2013, natimiza miaka 13 toka nianze kazi ya
muziki, namshukuru Mungu, umma wa Tanzania kwa kuendelea kusapoti muziki
wa Tanzania na kunipa nguvu mimi kama msanii, hivyo napenda wajumuike
nami na kuendelea kuniunga mkono,” alisema.
Jaydee alisema kuwa uzinduzi wa albamu hiyo, unadhaminiwa na
runinga ya East Africa (EATV), ambapo atawaburudisha mashabiki wake kwa
kuimba nyimbo zake ambazo zilibamba miaka ya nyuma.
Uzinduzi na sherehe hizo utafanyika Mei 31, mwaka huu na
kuwataka wapenzi na mashabiki wake kujitokeza na kumuunga mkono.

Post a Comment