ad

ad

Roma, Madee, Nay wa Mitego wafunika Airtel Yatosha Mwanza.

WASANII wa muziki wa kizazi kipya ‘Bongo Fleva’ wamefunika kwa kutoa burudani ya nguvu kwenye kampeni ya ‘Airtel Yatosha’ kwa kuwapa raha maelfu ya wapenzi wa muziki huo waliofurika kwenye viwanja vya wazi vya Furahisha jijini Mwanza.

Kampeni hiyo ya siku mbili inayoendeshwa na Kampuni ya simu ya Airtel iliyofanyika katika viwanja hivyo, maelfu ya wananchi wa Mkoa wa Mwanza walipata ushuhuda wa Airtel 

Yatosha kwa kununua laini za simu za mkononi za kampuni hiyo na jinsi ya kutumia huduma ya internet, kuongea kwa kujiunga na kupata dakika nyingi za muda wa maongezi kwenda mitandao mingine kwa bei nafuu zaidi kwa laini moja tu ya Airtel.

Wasanii wa Bongo Fleva waliotoa burudani na kuwaacha hoi maelfu ya wananchi waliofurika kupitia vibao vyao vinavyotamba kwenye vituo mbalimbali vya redio na runinga hapa nchini ni pamoja na Juma Kassim ‘Sir Nature’ na kundi lake la Wanaume Halisi, Roma Mkatoliki, Madee na Ney wa Mitego.

Maelfu ya wananchi walioshuhudia kampeni hiyo waliweza pia kushuhudia vipaji vya uimbaji kutoka kwa vijana walioshindanishwa na waliojitokeza kucheza muziki wa Bongo fleva katika viwanja hivyo na kupata zawadi za laini na fulana za Airtel.

“Wananchi wengi wamekuja hapa kupata burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wa muziki wa Bongo fleva kama ulivyojionea, lakini pia wengi kwa sasa wanatumia mtandao wa Airtel, ikiwamo huduma hii ya Airtel Yatosha pamoja na kununua laini na kupatiwa maelezo ya jinsi ya kutumia huduma hii,” alisema msanii Ney wa Mitego.

Akizungumzia kampeni hiyo, Meneja Uhusiano wa Kampuni hiyo, Jackson Mmbando alisema kwamba tangu kuzinduliwa na kufanyika katika mikoa sita hadi sasa hapa nchini, kumekuwa na mapokeo na mafanikio makubwa kwa kuongeza wateja wanaotumia mtandao wa Airtel kupitia huduma zote.

Mfanyabiashara wa vituo vya kuuza mafuta, Barnabas Mathayo wa jijini Mwanza, alitoa ushuhuda wa kukubali huduma inayotolewa na Airtel katika mahojiano maalumu, akisema kwamba tangu kuanzishwa kampeni ya Airtel Yatosha, amekuwa akinunua kifurushi na kujiunga na kujipatia muda wa kutosha kufanya mawasiliano na ndugu, rafiki, wavuvi wanaonunua mafuta kwa ajli ya boti zao pamoja na wafanyabiashara mbalimbali kupitia mitandao yote kwa bei ile ile.
Kampeni hiyo inaendelea katika mikoa mingine na mwishoni mwa juma hili itahamia jijini Dar es Salaam kwenye viwanja vya Zakhem.
Powered by Blogger.