TAYO WA BBA AKANUSHA KUPEWA $350,000 NA BILIONEA
Tayo (kulia) akiwa na mshindi wa BBA 2014 Hotshots, Idris (kushoto).
Mshindi wa pili wa BBA Hotshots, Tayo kutoka Nigeria amekanusha
habari zilisambaa wiki hii kuwa amezawadiwa $350,000 na bilionea wa
Nigeria, Ayiri Emani baada ya kuzikosa $300,000 za BBA zilizonyakuliwa
na Idris wa Tanzania.Tayo amekanusha habari hizo alipohojiwa na kituo cha Radio 1 South Africa. Amesema kuwa habari hizo za kupewa kiasi hicho kikubwa cha pesa na huku hata hamfahamu bilionea huyo, zimemletea usumbufu kwasababu watu wengi watadhani yeye ni milionea na huku sio kweli.
Tayo aliongeza kuwa yeye na Idris ni marafiki na anatarajia kuja Tanzania mapema iwezekanavyo.
(CHANZO: BIG BROTHER AFRICA 2014)
Post a Comment