ad

ad

ZITTO AICHAKAZA CHADEMA LEO HII



 
MBUNGE wa jimbo la Kigoma mashariki Zitto Zuberi Kabwe amekigalagaza Chama chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Baada ya kuibuka mshindi katika kesi iliyosomwa na Jaji wa mahakama kuu John Mtalemwa jijini Dar.

 Tukio hilo limetokea mapema leo ambapo Zito aliwasilisha shauri la kudai mahakama iwazuie kamati kuu ya chadema (CC) kumjadili kuhusu hatima ya Ubunge wake na kuhusiana na kuvuliwa kwa nyazifa zake mwishoni mwa mwaka jana

 Mahakama kuu imeamua kuwa Zitto ataendelea kuwa Mwanachama hai wa Chadema mpaka itakamalizika kesi ya awali inayodai Chadema kumrejeshea nyazifa zake za uongozi ndani ya Chadema ambapo haki zote za Zitto ndani ya chama chake zitakuwa chini ya uangalizi wa mahakama mpaka kesi itakapomalizika na kutolewa hukumu

Zitto alifungua kesi ya kudai kurejeshewa nyazifa zake ambazo alinyang’anywa mwishoni mwa mwaka jana, kesi hiyo iliambatana na kesi nyingine aliyoifungua hivi karibuni akidai kamati kuu isimjadili mpaka itakapoisha kesi yake ya awali na leo Mahakama kuu imempa ushindi Zitto na kuitaka Chadema na kamati zake zote kutomjadili Zitto


Kesi ya Zitto ya awali ya Zitto kudai nyazifa zake itaunguruma tena mapema februari 13, mwaka huu.
Powered by Blogger.