Usalama waimarishwa wakati wa kuapishwa Uhuru Kenyatta siku ya kesho.
Jeshi la Polisi nchini Kenya limetoa tahadhari kufuatia kuwepo kwa
taarifa za kufanyika maandamano makubwa ya makundi ya watu kutoka maeneo
tofauti nchini humo.
Uhuru Kenyata anatarajia kuapishwa kesho tarehe 09.04.2013. Kutoka mjini
Nairobi Sudi Mnette amezungumza na Emanuel Kisiangani ambaye ni mtafiti
mwandamizi kutoka katika taasisi ya masuala ya usalama (ISS) na kwanza
alitaka kujua kuna uwezekano wa kufanyika maandamano makubwa nchini
humo? Kusikiliza mazungumzo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo
chini.

Post a Comment