Serikali ya DRC na M23 warudi tena kwenye mazungumzo.
Wiki tatu baada ya kusitishwa kwa mazungumzo ya amani kati ya waasi wa
M23 na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wajumbe kutoka
pande zote mbili zinazozozana wamerudi mjini Kampala kuanzisha tena
mazungumzo.
Hata hivyo, waasi wa M23 wanailaumu serikali kwa kutumia mazungumzo ya
amani ya Kampala kujiandaa kwa vita na kuilaghai jumuiya ya kimataifa.
Mwandishi wetu wa Kampala Leylah Ndinda na taarifa zaidi. Kuiskiliza
taarifa hiyo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Post a Comment