Raia 37 elfu wa J/Afrika ya Kati wakimbilia nchi jirani.
Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR,
limetangaza kwamba, tangu mwezi Disemba mwaka jana hadi sasa, zaidi ya
raia 37 elfu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, wamelazimika kuyakimbia
makazi yao.
Shirika la Habari la Associated Press limemnukuu msemaji wa
shirika hilo Bwana Edrian Edwards akisema kuwa, karibu wakimbizi 31 elfu
wamekimbilia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo huku wengine wakikimbilia
nchi za Chad na Cameroon.
Edwards amesema kuwa, wengi wa wakimbizi hao
wanakabiliwa na hali mbaya hasa kutokana na kukosa mahitajio muhimu ya
kimaisha. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Shirika hilo kwa sasa
linajishughulisha na kutoa huduma kwa wakimbizi walioko nchini Kongo na
Chad huku wale walioelekea nchi nyengine wakiwa hawajapata msaada
wowote.
Post a Comment