Mapingamizi Yapigwa Chini Kinondoni, Mtulia na Mwalimu Sasa Kuchuana
MSIMAMIZI wa uchaguzi wa jimbo la
Kinondoni ambaye pia mkurugenzi wa manispaa hiyo, Aron Kagurumjuli
ameyatupilia mbali mapingamizi matatu yaliyowasilishwa na wagombea wa
vyama vya Chadema, CCM na CUF.
Baada ya jana ofisi ya msimamizi wa
uchaguzi kutoa barua ya utetezi kwa wagombea waliowekewa mapingamizi leo
Jumanne imetoa majibu ya kuyatupilia mbali mapingamizi hayo.
“Tumeyatupilia mbali mapingamizi yao kwa sababu hayana mashiko, kilichobaki ni wagombea kwenda uwanjani wakapambane,” amesema msimamizi huyo.
Post a Comment