ad

ad

Wananchi zaidi ya 200 Arusha hawana makazi baada ya nyumba zao kusombwa na mafuriko

Wananchi zaidi ya 200 katika kata sita wilayani Arumeru mkoani Arusha hawana makazi baada ya nyumba zaidi ya 60 kusombwa na mafuriko.
Mafuriko hayo ambayo pia yamesomba, Ng’ombe na Mbuzi zaidi ya 50 na kuku zaidi 120 ya meendelea kusababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu ya barabara jambo ambalo limeleta adha kubwa kwa wagonjwa na wajawazito ambao sasa wanalazimika kubebwa kwa mikono na machela kwenda kupata huduma.
 
Viongozi wa vijiji vilivyokumbwa na maafa hayo akiwemo Bw Onesmo Mollel amesema kuwa wameamua kuwashirikisha wananchi kuanza matengenezo ya awali katika barabara za mitaa mbalimbali ili ziweze kupitika na kuimba serikali kwasaidia korofi.
 
Akizungumza baada ya kutembelea maeneo hayo ya maafa, mkuu wa wilaya Arumeru Wilsoni Nkhambaku amewataka wote waliojenga maeneo ya mabondeni pamoja na wale wanaoishi katika mikondo ya maji kuondoka haraka ili kuepusha maafa zaidi.
 
Powered by Blogger.