ad

ad

Hope Lucy Ruhinda: Napenda Kuwa Na Mwanaume Asie Nipangia Aina Ya Mavazi Ya Kuvaa

Hope  Lucy  Ruhinda  ( 25 ) ni  mwanamitindo  anae  fanya  vizuri sana  katika  tasnia ya  urembo  nchini  Afrika.  

Mwanamitindo  huyu ambaye  ni  mtanzania  kwa  mama, na  mnyarwanda  kwa  baba, kupitia  kazi  zake  za  mitindo , ameonyesha  nia  ya  kufika  mbali  katika  tasnia  ya  mitindo., huku  lengo  lake   likiwa  kufikia  level  za  kimataifa  kama   Naomi  Campbell.

Akielezea  kuhus  safari  yake  katika tasnia  ya  mitindo,  Hope  anasema

“Tangu  nikiwa  shule  ya  msingi, siku   zote  nilikuwa  nikitamani  sana  kuwa muimbaji, dancer  au  mwanamitindo. Lakini  kwa  kuwa  sikuwa  na  kipaji  cha  kuimba  wala  kudance,  nikaamua  kujikita  katika  mitindo “

Akaongeza“ Nilipofika  O-Level  nikaanza  kufanya  modeling  for  fun.  Hapo  nilikuwa  bado  Tanzania. Nilipo maliza  O-Level  huko  Tanzania, nilikuja  kujiunga  na  masomo  ya  A-Level  katika  shule ya  sekondari   ya  FAWE Girls’  Secondary  School  hapa  Kigali.”

Nilipo maliza  A-Level nilienda  kushiriki  Miss  Rwanda, baada  ya  kushauriwa  na  kushawishiwa  na  rafiki  zangu  wa  karibu.  Mwanzoni  nilikuwa  mgumu  kukubali  ushauri wao, lakini  baada  ya  kutafakari  kwa muda, nikaamua  kushiriki.  
Kwenye  mashindano  sikufanikiwa  kuchukua  taji  la  Miss  Rwanda, Nililia  sana  siku  hiyo.  Sababu  kuu  ya  kushindwa  kwangu, walitaka  mtu anaye weza  kuzungumza  Kinyarwanda  fluent, na  mimi  sikuwa  na  uwezo  huo.

Hata  hivyo, shindano  la  Miss  Rwanda  lilinipa  exposure  kubwa  sana. Baada  ya  kuniona,   baadhi  ya  wadau  wa  masuala  ya  mitindo, walinishauri  niingie  kwenye  mitindo.

So  show  ya  Rwanda  Cultural  Fashion  ilipoanza, mwaka  2013  nilijiandikisha na  kushiriki  na kufanya  vizuri  sana.

Niliingia  kwenye  modeling  ili niweze  kublend it na  business. Nina  ndoto za  kuwa  mfanya  biashara  mkubwa, ndio  maana  ninasoma  biashara  pale University  Of  Kigali

Hope  anawashauri  wanamitindo  wafanye  kazi kwa kujituma  na  wawe  wajanja  wa  kutafuta  na  kuzitumia  fursa mbalimbali za  mitindo, kwani  modeling  ni  kazi  kubwa  yenye  fursa  nyingi sana  za  kibiashara.

Ana amini  kuwa  kujulikana  “ exposure’ ni hatua  kubwa  sana  kwa  mwanamitindo  kuweza kupata  nafasi ya  kupata  deals  na  endorsements
Pamoja  na  kwamba, ana  ndoto  za  kuwa  mfanyabishara  mkubwa, lakini  ana amini pesa  si  kila  kitu. Kwake  yeye  kuwa  na  hekima  ni  bora  kuwa  na  pesa  na  mali  nyingi. “ Maarifa  hudumu   daima  milele  lakini, pesa  na  mali  huweza  kuisha  na  kutekeketea  wakati  wowote.

Akitoa  maoni  na mtazamo wake  kuhusu  wanaume  anasema “  Wanawake hatuwezi kuishi  bila  wanaume. Vile  vile, wanaume  hawawezi  kuishi bila  wanawake. Hii ndio  sababu  Mungu  aliwaumba  Adam  na  Eva

Kuhusu  aina  ya  mwanaume   anaye mpenda , Hope  anasema :

“ Napenda  niwe  na  mwanaume  ambaye  hanipangii  aina  ya  mavazi  ya  kuvaa.  Pesa  na  muonekano, havina  umuhimu wowote  kwangi,  ili mradi tu ninaishi  maisha  huru  ya bila  kuwa  na  stress. “

Kuhusu  aina  ya  kifo  ambacho  atapenda afe,  Hope  anasema, “ hakuna  mtu  asie  ogopa  kufa, lakini si njambo  baya  kuomba  kifo  chema, na mimi  katika  hilo, ninamuomba  Mungu, siku yangu  ikifika  nife  nikiwa  usingizini.

Kuhusu  asicho kipenda, Hope  anasema  hapendi  uchafu,. Anachukizwa  sana  na  uchafu. Usafi  ndio  kila  kitu  kwangu, hata  nilipo kuwa  Fawe  Girls, nilipewa  cheti cha  kuwa   mwanafunzi msafi.

 Mbali na  mitindo, Hope  anajishughulisha  na  kazi  mbalimbali  za  kijamii, huku  akipenda  zaidi  kuwasaidia  watu w asio  jiweza  na  wanaoishi  katika  mazingira  magumu.

“ Huwa  ninafarijika  sana  moyoni, ninapo  ona  mtu  Fulani amelala  usingizi  mzuri  na  wa  amani, kwa  sababu  ya  msaada  nilio mpa.

No comments

Powered by Blogger.