ad

ad

HII KALI, ETI SIMBA WALICHEZA NA TOTO NDANI YA BWAWA


Mvua kubwa iliyonyesha juzi Jumamosi jijini Mwanza, ilitibua mipango ya Simba ya kuondoka na pointi tatu ilipopambana na Toto Africans kwenye Uwanja wa CCM Kirumba.

Katika mchezo huo, Simba ilikuwa mgeni wa Toto na matokeo ya mwisho yalikuwa sare ya bao 1-1, bao la Simba lilifungwa na Danny Lyanga dakika ya 22 huku Toto ikisawazisha kupitia kwa Evarist Benard katika dakika za nyongeza baada ya zile tisini kumalizika.


Baada ya mchezo huo, Kocha wa Simba, Muingereza, Dylan Kerr, amesema mchezo huo haukupaswa kuchezwa siku hiyo kutokana na uwanja kujaa maji, lakini anashangaa mwamuzi aliamuru uchezwe.

“Kabla ya kuanza kwa mchezo, mwamuzi alisema ataukagua uwanja kwa kudundisha mpira kama unadunda mechi ichezwe na kama haudundi basi iahirishwe kama sheria za soka zinavyosema.

“Lakini tunashangaa hakufanya hivyo na badala yake akaruhusu mechi ichezwe, hii haipo sawa kabisa na huku ni kuvunja sheria za soka kwani sheria hizo zipo wazi na kila mmoja anazifahamu.



“Ni wazi mashabiki walikosa ladha ya mchezo kabisa. Kutokana na masuala ya soka yanavyoendeshwa hapa nchini naamini soka la hapa halitiliwi maanani hata kidogo, haiwezekani mnacheza mpira huku viatu vimefunikwa na maji, sasa hapo mtachezaje kama siyo kuchoshana tu?
Powered by Blogger.