ad

ad

MNIGER WA YANGA MAMBO SAFI, TAYARI APEWA MAKAZI JIJINI DAR


Wakati Simba ikiwa kwenye mvutano na kiungo wake raia wa Zimbabwe, Justice Madjavi, kuhusiana na suala la kutompa nyumba ya kuishi, upande mwingine Yanga inaonekana haina shida na suala linaloitwa nyumba kwa wachezaji wake, kwani imempatia nyumba nzuri ya kuishi kiungo mpya Mniger, Issofou Boubacar Garba, iliyopo maeneo ya Shekilango jijini Dar.

Yanga ilimsajili Boubacar katika usajili wa dirisha dogo kwa lengo la kuziba nafasi ya kiungo Mbrazil, Andrey Coutinho waliyemfungashia virago vyake hivi karibuni.

Katibu wa timu hiyo, Dk Jonas Tiboroha, amesema kuwa, wamempatia nyumba mchezaji huyo maeneo ya Shekilango ikiwa inajitegemea.

“Kwa kawaida yetu Yanga huwa tunawapatia nyumba wachezaji wetu wote wa kimataifa tunaowasajili na hakuna hata mmoja anayekaa hotelini, ili kuweza kuepuka usumbufu wa hapa na pale.


“Kila mtu anapatiwa nyumba yake na kama itatokea watakaa nyumba moja, basi ‘apartment’ tofauti, hakuna anayekaa sehemu moja na mwenziye, tumempatia Mniger nyumba maeneo ya Shekilango ila hatuwezi kusema tumempangia kwa kiasi gani, hiyo ni siri yetu,” alisema Dk Tiboroha.
Powered by Blogger.