Kapombe: Naumwa, nipo tu nyumbani Moro
BEKI aliyekuwa akikipiga AS Cannes ya Ufaransa,
Shomari Kapombe, amesema ameshindwa kufanya mazoezi kwa kuwa amekuwa
akisumbuliwa na malaria mara kwa mara.
Awali beki huyo alikuwa akicheza Simba na alikwenda kuichezea AS
Cannes lakini amesema kwa sasa anatumia muda wake mwingi akiwa Morogoro
akijiuguza.
Akizungumza beki huyo ambaye
inadaiwa yupo kwenye hatua za mwisho kukamilisha usajili wa kutua Azam
FC, alisema kwa sasa anashinda tu nyumbani kutokana na kusumbuliwa na
malaria kiasi kwamba hajielewi.
“Kwa sasa nipo tu Morogoro nashinda nyumbani kutokana na kusumbuliwa
na ugonjwa wa malaria, ugonjwa huu umesababisha mimi kushindwa kufanya
mazoezi kabisa ili kuweza kuendelea kulinda kiwango changu.
“Ndiyo maana sipendi kuzungumzia masuala ya soka kwa sasa, kwa
anayetaka kufahamu naelekea timu gani amuulize wakala wangu ndiye
atamuelekeza kila kitu anachohitaji, mimi sina cha kuongea kwa sasa,”
alisema Kapombe.

Post a Comment