ad

ad

SAHAU LIONEL MESSI, XAVI NDIYE ALIYEIBEBA BARCELONA DHIDI YA PSG


WENGI wameelekeza fikira zao kwamba kuingia dimbani kwa Lionel Messi kipindi cha pili ndiko kumeibeba Barcelona dhidi ya Paris Saint Germain (PSG), usiku wa Jumatano, lakini ukweli unabaki kuwa ni Xavi ndiye aliyekuwa na mchango mkubwa, huku akiandika rekodi ya kugawa pasi dimbani.

Barcelona ililazimika kufanya kazi ya ziada kupata nafasi katika nusu fainali ya Champions League.
Iliwekwa nyuma baada ya dakika 50, lakini ikafanikiwa kupenya kwa sheria ya mabao ya ugenini pale Pedro aliposawazisha na kufanya sare ya 1-1 dakika ya 71. Timu hizo zilitoka 2-2 mechi ya kwanza Ufaransa.

Xavi mwenye miaka 33 alicheza dakika zote 90 za mechi hiyo kwenye dimba la Nou Camp, na alifanikiwa kwa asilimia 100 kusambaza mipira kwa wachezaji wenzake dimbani, ambapo alipiga jumla ya pasi 96, ambapo hakuna hata moja iliyopotea njia.

Kuna wachezaji wengi waliong’ara kwa kugawa pasi kwa usahihi kwenye Champions League katika kipindi cha miaka 10 tangu msimu wa 2003/04, lakini hakuna aliyewahi kufanya hivyo kwa asilimia 100. 
Kabla ya ‘maajabu’ ya Xavi, orodha ya ukamilifu wa pasi ilikuwa ikiongozwa na Javier Zanetti aliyefanya hivyo kwa asilimia 72 katika mechi kati ya Inter Milan na Tottenham miaka mitatu iliyopita.

Orodha kamili ya nyota wanaoongoza kwa kupiga pasi kwa ukamilifu tangu mwaka 2003; asilimia zao, mechi na miaka kwenye mabano ni: Xavi (96% - Barcelona v PSG, 2013); Javier Zanetti (72% - Inter vs Tottenham, 2010); Emmanuel Eboue (54% - FC Porto vs Arsenal, 2006); Lilian Thuram (50% - Barcelona vs Stuttgart, 2007) na Cristiano Ronaldo (50%, Real Madrid vs Man City, 2012).

Wengine ni Paulo Vinicius (48% - Braga vs Galatasaray, 2012); Martin Caceres (48% - Basel vs Barcelona, 2006); John Terry (47% - Chelsea vs Werder Bremen, 2008); Rolando Jorge Pires da Fonseca (45% - FC Porto vs Dynamo Kiev, 2006); Ivan Helguera ( 43% - Roma vs Real Madrid, 2004) na Sergio Ramos (43% - Real Madrid vs Dinamo Zagreb, 2011).
Via saluti5.com
Powered by Blogger.