ad

ad

Mbunge ahoji wananchi kuzuiwa kuvua samaki

JIBU LA SWALI LA MBUNGE Bukoba vijijini
MBUNGE wa Bukoba Vijijini, Josson Rweikiza (CCM), amehoji mpango wa serikali wa kuwazuia wananchi kuvua samaki katika Ziwa Victoria na kusema kuwa kufanya hivyo ni sawa na kuwanyima haki.


Rweikiza alihoji mpango huo bungeni jana alipokuwa akiuliza swali la msingi, alihoji kwa nini serikali isiwaruhusu wananchi kuvua samaki katika maeneo mengine au kwa wakati usiokuwa wa mazalio ya samaki.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Benedict ole Nangoro, alikanusha taarifa hiyo na kusema wananchi wanaoishi kandokando mwa Ziwa Victoria hawajawahi kuzuiwa kuvua samaki wa kitoweo wala wa biashara, bali wamehimizwa kuzingatia uvuvi endelevu kwa mujibu wa sheria ya taifa ya uvuvi ya mwaka 1997.
Pia alisema kanuni husika zinazosimamiwa na serikali zimeainisha aina ya zana zinazoruhusiwa kutumika kuvua aina mbalimbali za samaki.

Alifafanua kuwa kanuni Na. 58(1)(b) inakataza kuvua, kushusha, kumiliki, kusafirisha nje ya nchi au kufanya biashara ya sato wenye urefu chini ya sentimenta 25.
Aidha, alisema kanuni ya 66(1)(k) inakataza kumiliki, kutumia na kusababisha mtu kutumia kwa uvuvi wa dagaa nyavu zenye macho chini ya milimita nane.
Naibu Waziri huyo alisema serikali inawahimiza wananchi kutumia zana halali kama sheria na kanuni za uvuvi zinavyoelekeza.
Powered by Blogger.