ad

ad

HIV: KWANINI UPIME? (Faida za Kupima HIV.)

Daktari siko tayari kupima labda mpaka mwakani;Hapana doctor heri nife kuliko kupima HIV.Hayo ni baadhi ya majibu unayopata unapomshauri mgonjwa kupima HIV. Kuna sababu nyingi zinazowafanya wagonjwa kutokuwa tayari kupima maambukizi ya VVU. Mojawapo ni woga kwani kwa watu wengi kuwa na maambukizi ya VVU ni sawa na kifo. Sababu nyingine ni baadhi ya wagonjwa kuamini kuwa baadhi ya watoa huduma wamekuwa na tabia ya kutoa siri za wagonjwa kwa watu wasiohusika.

Hata hivyo ukiweka hizo sababu kando,kuna faida kubwa za kuweza kukusukuma kufanya maamuzi ya kupima leo. Afya njema ni jukumu la kila mmoja wetu na hivyo tunawajibu wa kutunza na kujua hali za afya zetu. Zifuatazo ni faida za kupima HIV.

Kujua hali ya afya.
Ni vizuri ukipima HIV kwani ndio njia pekee ya kujua kama una maambukizi au laa. Watu wanaonekana kuwa wazima kabisa wanaweza kuwa wanavirusi vya UKIMWI katika miili yao. Ukiitambua hali ya afya yako utachukua hatua sahihi kulingana na hali uliyonayo .

Kumkinga mwenziwako na wengine
Baada ya kupima HIV na kujua hali yako ya afya itakusaidia kumkinga mwenziwako pamoja na wengine mlionao katika mahusiano. Ni wajibu wako kuhakikisha kuwa ulionao katika mahusiano hawapati maambukizi. Ni vyema ukiwalinda hasa kwa kutumia kondomu.

Kujikinga usipate maambukizi mapya
Iwapo utachukua jukumu la kupima itakusaidia kujikinga usipate maambukizi mapya. Kama utakuwa una VVU,maambukizi mapya yatachochea kuzaliwa kwa aina nyingine(strain) ya virusi ambayo inaweza kuwa sugu au kushambulia kinga kwa haraka zaidi

Kuanza matibabu mapema
Huwezi kuanza matibabu kama hujui hali yako. Tafiti mbalimbali zimeonesha faida za kuwahi kuanza matibabu. Hii itasaidia kupunguza hatari ya kupata magonjwa nyemelezi.


Hivyo basi ni vyema kuamua na kuchukua hatua leo ya kupima. Kuna vituo mbalimbali vinavyotoa huduma ya ushauri na kupima.
 
Powered by Blogger.