ad

ad

Mchezaji soka wa Scotland atiwa mbaroni kwa tuhuma za kuiba ndani ya 'supermarket'

Leigh Griffiths mshambuliaji machachari na mtambo wa kupachika mabao wa  klabu ya soka ya Hibernian nchini Scotland ametiwa mbaroni baada ya kupatikana akiiba kwenye duka la Tesco mjini Edinburgh. Griffiths alitiwa mbaroni na walinzi wa duka hilo.
Polisi ya Scotland imethibitisha juu ya kutokea tukio hilo la kutiwa mbaroni mshambuliaji wa klabu ya Hibernian mwenye umri wa miaka 22. Hata hivyo Polisi imeeleza kuwa, Leigh atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo katika siku zijazo. Polisi imeeleza kwamba uongozi wa klabu yake umeshapewa taarifa juu ya tukio la mchezaji wao, ingawa wamesema kwamba suala hilo liko mikononi mwa polisi.

Griffiths ambaye alichukuliwa kwa mkopo kutoka klabu ya Wolverhampton Wanderers  tayari ameshaipachikia timu yake mabao 15. Mchezaji huyo alianza kuvaa jezi ya timu ya taifa ya  Scotland mwaka jana wakati iliposhuka dimbani dhidi ya  Luxembourg mwaka jana.
Powered by Blogger.