ad

ad

Mahakama Kenya yatupilia mbali kesi zilizopinga ushindi wa Kenyatta

Jaji Mkuu, David Maraga.
Mahakama ya Juu Kenya imetupilia mbali kesi mbili zilizokuwa zimewasilishwa kupinga uchaguzi wa marudio, na hivyo imeidhinisha ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta.

Jaji Mkuu David Maraga amesema majaji kwa kauli moja wameamua kwamba kesi zote mbili hazina msingi.  Kesi ya mbunge wa zamani Bw Harun Mwau na wanaharakati wawili Njonjo Mue na Khelef Khalif zimetupiliwa mbali.

“Uchaguzi wa 26 Oktoba umedumishwa, sawa na ushindi wa Bw Kenyatta. Kila upande utasimamia gharama yake,” amesema.
Uamuzi wa kina utatolewa katika kipindi cha siku 21.

No comments

Powered by Blogger.