Mfalme wa Swaziland Aoa Mke wa 14, Mtoto wa Waziri Wake
MFALME Mswati wa Tatu wa
Swaziland kwa mara nyingine ameongeza idadi ya wanawake kwa kuoa
mwanamke mwingine. Katika kuadhimisha Ngoma ya Umhlanga ambayo hufanyika
kila mwaka kwa kumpa mfalme fursa ya kuchagua mwanamke wa kuoa, mfalme
huyo hivi karibuni alimchagua Siphele Mashwama mwenye umri wa miaka 19
kuwa mkewe wa 14.
Msichana huyo ambaye ni binti wa waziri Jabulile
Mashwama katika serikali ya nchi hiyo, alipewa manyoya maalum mekundu ya
ndege anayejulikana kama emagwalagwala ambaye huhusishwa na sherehe
hiyo maalum ya kifalme. Mswati ambaye ana umri wa miaka 49 huchagua
wanawake waliovuka umri wa miaka 19.
Pamoja na talaka kupigwa marufuku katika nchi
hiyo ya kifalme, Mfalme Mswati amewahi kuwataliki wake zake watatu.
Siphele ambaye ni mhitimu wa Waterford Kamhlaba World University
College, alifuatana na Mfalme Mswati alipohudhuria Mkutano Mkuu wa Umoja
wa Mataifa hivi karibuni.
Habari hiyo ilifichuliwa na msimamizi wa sherehe za kifalme, Hlangabeza Mdluli, aliyethibitisha kwamba Mswati alikuwa amefuatana na mkewe huyo ambaye kwa umri ndiye mdogo zaidi.
Wake
zake wengine ni pamoja na: Inkhosikati LaMatsebula, Inkhosikati LaMotsa,
Inkhosikati LaMbikiza, Inkhosikati LaNgangaza, Inkosikati LaMagwaza
(ameachika), Inkhosikati LaHoala (ameachika), Inkhosikati LaMasango,
Inkhosikati LaGija (ameachika).
Wengine ni: Inkhosikati
Magongo, Inkhosikati LaMahlangu, Inkhosikati LaNtentesa, Inkhosikati
LaNkambule, Inkhosikati Ladube na Inkhosikati LaFogiyane. Mfalme King
Mswati, anayejulikana pia kama Ngwenyama, yaani simba, anasemekana kuwa
na watoto zaidi ya 13 ambao ni pamoja na binti yake mkubwa zaidi aitwaye
Sikhanyiso, Sibahle Dlamini, Makhosothando Dlamini, Majaha Dlamini, na
Tiyandza Dlamini.
Wengine ni Sakhizwe
Dlamini, Saziwangaye Dlamini, Bandzile Dlamini, Lindaninkosi Dlamini,
Mcwasho Dlamini, Temtsimba Dlamini na Temaswati Dlamini, among others.
Baba yake Mswati, Mfalme Sobhuza wa Pili, alioa wanawake 70. Mswati
amekuwa akishutumiwa kwa kujilimbikizia utajiri wakati watu wake wengi
ni maskini.
Hivi karibuni, nchi hiyo ndogo ilitumia kiasi cha Dola milioni 2.2 (sawa na Sh. bilioni 5) kwa kununua magari ya anasa aina ya BMW 740i na pikipiki 80. Magari hayo yalikuwa ni kwa ajili ya viongozi wa Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa Afrikca (SADC) waliyoyatumia kwa ajili ya mkutano wa siku mbili.
Wakiwa kwenye sherehe za mavuno.
Wakiwa kwenye sherehe za mwaka.
Habari hiyo ilifichuliwa na msimamizi wa sherehe za kifalme, Hlangabeza Mdluli, aliyethibitisha kwamba Mswati alikuwa amefuatana na mkewe huyo ambaye kwa umri ndiye mdogo zaidi.
Wake wengine wa Mswati.
Wakiwa kwenye sherehe za mwaka.
Mswati akikagua gwaride.
Hivi karibuni, nchi hiyo ndogo ilitumia kiasi cha Dola milioni 2.2 (sawa na Sh. bilioni 5) kwa kununua magari ya anasa aina ya BMW 740i na pikipiki 80. Magari hayo yalikuwa ni kwa ajili ya viongozi wa Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa Afrikca (SADC) waliyoyatumia kwa ajili ya mkutano wa siku mbili.






Post a Comment