Leo Ndiyo Leo Nay wa Mitego, Barnaba Kukinukisha Dar Live
Akizungumza na Mikito Nusunusu, Nay alianza kwa kuwapongeza mashabiki wote waliofurika jana katika Viwanja vya Karume na kuwasihi moto uendelee kuwa huohuo siku ya leo wajitokeze kwa wingi.
“Nimefarijika sana, vijana wengi bado wanatamani burudani kutoka kwangu na leo (jana) ile ilikuwa rasharasha tu mvua ya mawe ipo kesho (leo) ndani ya Dar Live.
“Kwa zaidi ya miaka mitatu sijafanya shoo ya kishindo na safari hii itakuwa kiboko maana nimejiandaa vya kutosha kuwapa mashabiki kitu wanachopenda.
Nitapiga ngoma zote kuanzia Itafahamika, Helo, Muziki Gani, Muda Wetu, Pale Kati Patamu, Uko Kwenu Vipi hadi Shika Adabu Yako na Wapo,” alisema Nay.
Naye Mratibu na Meneja wa Dar Live, Juma Mbizo aliongezea kuwa usiku huo unaotambulika pia kama Usiku wa Wabishi, watakuwepo wakali kibao wanaotikisa katika vichekesho na Muziki wa Bongo Fleva.
Tamaa na Wana Ndoto,” alisema Mbizo na kuongezea; “Mashabiki wasiwaze kabisa kuhusu kiingilio kwani lengo ni kutoa shoo sawa na bure hivyo watalipia hela ya mboga yaani kiingilio kiduuuuuchu sana cha shilingi 5,000 tu kitakachomuwezesha kila mpenda burudani aweze kuhudhuria na kuimba Wapo pamoja na Nay jukwaa moja,” alimaliza Mbizo.
Post a Comment