ad

ad

NYUMA YA MACHOZI - 18


MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’

ILIPOISHIA:
Alikunywa kidogo bila kujua alikuwa amepangiwa mchezo mwingine katika soda, aliona kama inamchelewesha alikunywa yote ili awahi kuondoka. Lakini hakufanya lolote baada ya kupatwa na kuzunguzungu na kujilaza kwenye kochi bila kujua. Jamaa alimpigia simu Jimmy aliyekuwa nje ya hoteli.
SASA ENDELEA...
Jimmy aliingia ndani ya hoteli na kumkuta Kilole amejilaza kwenye kochi hakiwa hajitambui. “Ooh! Kazi nzuri sana,” alimpongeza mwenzake.
“Mmh! Nilikuwa kwenye wakati mgumu unajua kazi kama hujaifanya hata siku moja lazima utakuwa hujiamini, wasiwasi wangu anaweza kuja na polisi.”
“Aje na polisi hajitaki, vipi mzigo amekuja nao?”
“Huu hapo,” Joe alimpa bahasha lililokuwa na fedha. Kabla ya kufanya lolote walihesabu fedha na kukuta milioni tano taslimu, Jimmy alimkatia Joe milioni moja kama malipo ya kazi aliyompa.
“Mzee nafikiri zinakutosha.” “Asante mkuu, nini kinaendelea?”
“Bado sinema inaendelea, sasa hivi tutafanya naye mapenzi kwa zamu huku tukipiga picha ambazo naamini zitazidi kututengenezea fedha.”
“Hakuna tatizo.”
Walimbeba Kilole aliyekuwa hajitambui na kumlaza kitandani kisha walimvua nguo zate na kuanza kumbaka kwa zamu huku wakimpiga picha za aibu. Baada ya kumaliza zoezi la aibu waliondoka na kumwacha Kilole akiwa amelala hajitambui.
********
Majira ya mchana Teddy alimpigia simu Mr Deus kutaka kujua kama ana nafasi waonane kutokana na baadhi ya washirika wake jioni ya siku ile kuwa na safari kufuata mzigo. “Haloo brother za kazi?” “Nzuri, sijui zako.”
“Zangu ziko poa, samahani tunaweza kuonana mchana huu?”
“Hakuna tatizo.”
“Basi njoo mara moja nikukutanishe na jamaa zangu ili tuianze kazi mara moja.” “Hakuna tatizo, tutakutana wapi?”
”Njoo na gari mpaka sehemu uliyoniacha siku ile.”
“Hakuna tatizo ndani ya robo saa nitakuwa hapo.”
“Okay, baadaye.”
Deus alikata simu na kujiandaa kwenda kuonana na kundi la wauza madawa ya kulevya. Baada ya kupanga vitu katika hali nzuri alitoka na kumuaga msaidizi wake.
“Happy natoka kidogo.” “Hakuna tatizo bosi.” Mr Deus alielekea kwenye maegesho kuchukua gari lake na kuelekea kwenye wito, alipofika eneo aliloelezwa alilipaki gari pembeni ya barabara kusubiri maelekezo. Baada ya muda simu yake iliita, alipoitazama alikuta ni Teddy, alibofya cha kupokelea na kuweka sikioni.
“Haloo.” “Haloo nimekuona, teremka kwenye gari lako na kupanda kwenye gari litakalo simama mbele yako.”
“Na gari langu?” “Liache tu litakuwa katika usalama wa hali ya juu, kwa hilo usihofu.”
“Okay,” Mr Deus alikata simu na kuteremkana kulifunga gari lake na kufuata maelekezo. Kabla hajapiga hatua Range Rover Vogue nyeusi yenye vioo visivyoonesha ndani ilisimama mbele yake na kufunguliwa mlango.
Hakupoteza muda aliingia ndani ya gari na kufunga mlango na gari liliondoka. Ndani ya gari kulikuwa na watu watatu Teddy aliyekuwa akiendesha gari na wanaume wawili waliokuwa wamekaa siti za nyuma.
“Habari zenu?”
“Nzuri,” Walijibu kwa mkato.
“Samahani brother,” Teddy alisema huku akipaki gari pembeni. “Bila samahani.”
“Naomba ufuate utaratibu wetu kabla ya kufika kwetu.”
“Hakuna tatizo.” “Utafungwa kitambaa usoni mpaka tutakapofika.”
“Hakuna tatizo mnaweza kufanya.”
Baada ya kukubali alifungwa kitambaa cheusi usoni na safari iliendelea bila kujua anapelekwa wapi. Baada ya dakika tano gari lilisimama na kuombwa
Mr Deus aliteremke, alitii amri na kuteremka kisha alishikwa mkono na kuongozwa hadi sehemu na kufunguliwa kitambaa usoni.
Baada ya kufunguliwa alijikuta yupo mbele ya sebule lililokuwa na kila kitu cha thamani. Ndani ya sebule ile kulikuwa na watu zaidi ya nane ukijumlisha watatu aliokuja nao wakawa jumla watu kumi na mbili pamoja na yeye mwenyewe.
“Karibu Mr Deus jisikie huru, ila samahani kukuleta kama mateka.”
“Kawaida tu wala hakuna baya.”
“Karibu kwenye kochi.”
“Asante,” alijibu huku akikaa kwenye kochi, baada ya kuketi aliwasalimia aliowakuta.
“Habari zenu.”
“Nzuri,” Waliitikia kwa pamoja.
“Mr Deus hawa ndiyo washirika wangu, huyo hapo ni Mateez anayefuata Sopas, Natalie, Suzy, Moops, Sweet, Pako, Flog, JMS na Poona, nina imani mimi unanifahamu?”
Mr Deus alikubali kwa kutikisa kichwa. “Waungwana huyu ndiye mtu niliyewaeleza ana umuhimu mkubwa kwetu, nimeweza kumwelewesha na kanielewa. Kwa vile kazi hii haihitaji kupoteza muda nina imani kuanzia muda wowote biashara ifanyike.
“Mr Deus hawa ndiyo washirika wangu niliokueleza kwa bahati nzuri tumekutana sehemu kubwa ya kundi letu. Wengine watatu utawajua kwa vile wiki ijayo wanaingia nimezungumza nao ili wapitie katika mikono yako salama japo wawili wamesema wataanza baada ya sisi ila mmoja atakuja na mzigo ndogo kujaribu.”
“Hakuna tatizo kazi itafanyika vizuri kila mmoja ataifurahia,” alisema Mr Deus baada ya kumsikiliza Teddy.
“Kwa hiyo kazi rasmi inaanza mwezi ujao kwa mwezi una uhakika wa kutengeneza zaidi ya bilioni mbili.”
“Hakuna tatizo nina imani mtafurahia kufanya kazi pamoja japo ni ya hatari.”
“Baada ya makubaliano hayo, tunakuonya tena kosa lolote la kizembe litagharimu uhai wako,” Teddy alitoa onyo lingine.
“Najiamini kuliko mnavyonidhania,” Mr Deus aliwatoa wasi.
“Kumbuka nilikukataza usimwambie siri hii hata mkeo.”
“Siwezi kumwambia mtu.”
Baada ya mazungumzo Mr Deus aliagwa na kupewa asante wa kukubali kufanya kazi na kundi lile ya milioni 55 kwa kila mmoja kutoa milioni tano. Baada ya mazungumzo yale alifungwa tena kitambaa na kurudisha hadi kwenye gari lake na kumkabidhi huku wakimuacha Mr Deus akiwa hajui alikuwa wapi.
******
Kilole alishtuka na kujishangaa yupo wapi baada ya kushtushwa na mazingira aliyoyaona mbele yake. Alijiuliza pale amefikaje na anafanya nini, kingine kilichomshtua ni kujikuta kitandani akiwa mtupu na pembeni yake kulikuwa na kondomu zaidi ya nne zilizotumika.
Alishtuka na kujishika sehemu za siri na kukuta kweli amebakwa, pembeni yake kulikuwa na bahasha mbili zilizokuwa imeandikwa jina lake. Kabla ya kuichukua ile bahasha alitulia na kuvuta kumbukumbu ya kufika pale. Alikumbuka alipeleka milioni tano ili apewe picha alizipiga akifanya mapenzi na Kinape. Aliendelea kuvuta kumbukumbu na kukumbuka baada ya kuonana na yule kijana alikaribishwa soda lakini kilichoendelea hakujua mpaka aliposhtuka na kujikuta akiwa mtupu kitandani huku ikionesha amebakwa zaidi ya mara nne kutokana na mipira minne ya kiume iliyotumika.
Alijipa ujasiri na kunyanyuka hadi bafuni na kuoga kisha alirudi chumbani na kuvaa nguo zake kisha alichukua bahasha mbili zilizokuwa na jina lake na kuziweka katika mkoba wake na kutoka nje ya hoteli kurudi nyumbani kwake.
Alipofika nje ilionesha kiza kilikuwa kimeingia, alitoa simu yake kwenye mkoba na kuangalia saa ilimuonesha ni saa mbili usiku. Alijikuta akishtuka na kujiuliza utamueleza nini mume wake, katika simu yake kulionesha kuna simu zilizopigwa zaidi ya mara kumi za mume wake pamoja na Kinape.
Japo roho ilimuuma kwa kitendo cha kinyama alichofanyiwa na kuapa kulipa kisasi, lakini aliweka pembeni maumivu yale na kutafuta njia ya kukabiliana na mumewe nyumbani atakayetaka kujua alikuwa wapi. Lakini ilikuwa tofauti na alivyofikiria, alipofika nyumbani alishangaa kukuta mumewe hajarudi. Mfanyakazi wa ndani alipomuuliza alisema hajarudi, ile ilimpa nguvu na kumpigia simu mumewe. “Haloo sweet.”
“Ooh! Honey vipi mbona napiga simu hupokei mpenzi, kuna nini?”
“Nilikuwa nimelala kichwa kimeniuma ghafla.”
“Nilitaka kukujulisha kuwa nitachewa tuna kazi moja nzito.”
“Mmh! Mume wangu, siyo unanila kisogo,” Kilole alijifanya kulalamika.
“Mke wangu siwezi kutoka nje ya ndoa yangu nakupenda sana, hasa mwenetu ambaye ndiye mrithi wetu na yote nayafanya kwa ajili yenu.”
“Asante mume wangu, nashukuru kusikia hivyo.” “Nikimaliza tu narudi nyumbani.”
“Nakutakia kazi njema, nakusubiri kwa hamu,” Kilole alizidi kumtia ujinga mumewe. Baada ya kukata simu aliingia chumbani mwake na kuziangalia zile bahasha, bahasha ya kwanza ilikuwa na picha alizopiga akifanya mapenzi na Kinape. Bahasha ya pili kulikuwa na picha ambazo zilimmaliza nguvu lakini akijikaza na kuendelea kuzitazama.
Alijiona akibakwa na wanaume wawili, alishtuka na kukumbuka soda aliyokunywa ndiyo ilimfanya apoteze fahamu na kumfanya yule mwanaume na mwenzake wambake.
Roho ilimuuma kutoa milioni tano bado wamembaka na kumpiga picha chafu. Ndani ya bahasha kulikuwa na karatasi iliyokuwa na ujumbe usemao;
Kwa vile unapenda mchezo huo, baada ya kukupa picha zako na kutupa milioni tano, picha hizo zingine zinataka milioni kumi, la sivyo siri ilimfikia mumeo. Tutakupigia simu kujua utatupa lini na wapi?
Kilole jasho lilimtoka na kuona kama laana ya matendo yake ndiyo inayomtafuna, alijiuliza milioni kumi akiwapa lazima watatengeneza mpango mwingine. Wasiwasi wake huenda mpango ule Jimmy anaujua, lakini hakutaka kutumia pupa zaidi ya kutumia hata kishawishi cha fedha ili Jimmy amsaidie. Wazo lingine lilikuwa kumuwahi Deus kabla hajajua lolote kwa kumuua ili kuepusha aibu, lakini wazo la kuua bado hakulipa nafasi kutokana na Kinape kuweka pingamizi. Akiwa amechanganyikiwa simu yale iliita, aliipokea na kusema:
“Haloo.”
“Haloo, bahasha umeiona?”
”Wewe nani?” “Mdau wako, nina imani ujumbe umeuona nieleze hizo fedha nitapata lini?”
”Lakini kaka yangu nimekukosea nini mpaka kunifanyia unyama kama huo?” Kilole alilalamika huku akimwaga chozi. “Hujadhalilishwa na mtu, biashara umeianza wewe, sisi tunaiendeleza.”
“Kaka yangu milioni tano nimekupa leo, hizo kumi nitazipata vipi?”
“Kama huna pa kuzipata basi salamu utazikuta kwa mumeo,” sauti ya upande wa pili ilimtisha.
“Msifanye hivyo, nioneeni huruma.”
“Hukujionea huruma sisi tutakuonea vipi?”
“Basi nipunguzieni.”
“Tulikuwa tunataka milioni hamsini, lakini nimepunguza mpaka kumi bado huoni huruma yangu.”
“Basi nipeni muda wa muda ili nizikusanye.”
“Tutakupa siku mbili.”
“Mbona ndogo?”
“Kama ndogo utajuana na mumeo tena tuinampa na za mwanzo ulizopiga na shemeji yako.”
“Basi nitawapeni, nakuombeni msimpe mtu.”
“Hakuna tatizo timiza haja zetu.”
“Hakuna tatizo.”
“Kwa heri, usiku mwema.”
Baada ya kukata simu alijikuta akirudiwa na maneno ya mtu aliyetaka fedha kwa kusema alifanya mapenzi na shemeji yake ile ilionesha kabisa Jimmy huenda mpango mzima anaujua. Kilole pamoja na kutokewa na tukio zito la kumdhalilisha huku likizidi kumuingiza kwenye mazingira magumu. Lakini hakutaka kuyumba kwani aliamini vita ile ni yake na yeye ndiye anayetakiwa kupambana mpaka tone la mwisho.
Alizirudia zile picha na kuuona unyama aliofanyiwa ikiwa pamoja na kuingiliwa kinyume na maumbile. Moyo ulimuuma sana na kujikuta akidondokwa na machozi kutokana na udhalilishwaji kama ule. Aliapa kupigana nayo mpaka hatua ya mwisho hata kwa mtutu kwani alikuwa anajua kutumia vizuri chombo cha moto baada ya kufundishwa na mumewe na kujua kuitumia vizuri.
Alikumbuka visasi vingi ambavyo ameviona kwenye sinema hutendeka usiku kwa mtu kuingia sehemu na kufanya mauaji kisha kutokomea bila mtu kujua.
Wazo lake lilikuwa kwenda kumbana Jimmy ili amtaje mtu mwenye picha zake na alipanga kuhakikisha anamuua Jimmy na kijana anayemtumia kama mtaji. Wakati akiwaza vile alishtuka kusikia mlango ukigongwa, alificha picha kwenye kabati na kwenda kufungua mlango.
Alifuta machozi na kujirudisha katika hali ya kawaida kisha alipofungua akijua mumewe karudi, lakini kumbe alikuwa Kinape ambaye alionekana mwenye jambo zito kichwani mwake kutokana na mwonekano wake. Kilole alizidi kuchanganyikiwa na hali ile ambayo aliona huenda inafanana na yake.
“Kilole mbona hivyo?” alimuuliza kwa mshangao. “Kilole umeniweka katika wakati mgumu sana,” Kinape alisema huku akikuna kichwa.
“Mungu wangu! Amejua? Kwa nini tusimmalizie mbali?”
“Tummalizie mbali nani?”
“Si Deus.”
“Kwa kosa gani?”
“Si amejua.”
“Wala si hilo.”
“Picha ameziona?”
“Kilole hebu acha papala, yote unayouliza siyo.”
“Sasa nimekuweka kwenye wakati mgumu kivipi?”
Tukutane Jumatatu

No comments

Powered by Blogger.