ad

ad

HADITHI: Msafara wa Mamba -15


MTUNZI: Ally Mbetu ‘DR AMBE’

ILIPOISHIA:...

ILIPOISHIA:
“ Kutokana na maelezo ya mwenzio kusikiliza habari za pembeni kuwa wewe ni muathirika japo mwanzo aliziba macho lakini imefikia kikomo sasa kwa hiyo una unafasi nyingine ya kudhigilisha ukweli."
"Lakini daktari si jana tu tumepima wote na kukutwa tupo salama sasa nashangaa tatizo nini?"
"Sikiliza mzee Joel kuna taarifa ambazo nina imani leo zitapata ukweli kuwa wewe una urafiki na madaktari wa hospital unayotibiwa hivyo kukufichia siri zako kwa kutoa majibu ya uongo."
"Nani kasema habari hizi za uuaji?" Anko macho yalimtoka pima.
SASA ENDELEA…

"Si wakati wa kutafuta mchawi vipimo ndivyo vitakavyo waonyesha wachawi wenu."
"Haya tupime."
Mshauri baada ya kuandika majina yetu tulikwenda chumba cha kupimia vipimo kisha tulirudi kwenye kiti tusubiri majibu ambayo yalichukua robo saa. Baada ya majibu kufika mbele ya meza nilishangaa kumuona Anko akijipekua kama amepoteza kitu. Alitoa pochi yake na kutoa noti ya elfu kumi na kunipa
"Herena niletee vocha ya simu mara moja."
"Mwache tu nitamtuma mtu afuate," mshauri aliingilia kati mzungumzo.
"Hapana, kwenye pesa huwa simuamini mtu, wacha tu my daring afuate."
Sikutaka mabishano nilinyanyuka na kutoka nje ya kituo kwani maduka hayakuwa mbali. Nilinunua haraka na kurudi ndani, nilishangaa mjomba alinyamaza ghafla baada ya kuniona na kuniuliza.
"Vipi umepata?"
"Ndiyo."
"Vizuri, samahani mpenzi nilisahau kukuagiza ya elfu 20 naomba umenilee nyingine."
"Dear hebu kwanza tusikilize majibu mara moja nyingine tutanunua tukitoka."
"Mwache tu kwanza si unajua kuna wateja wengine tumewagandisha kwa kipindi kirefu kwa ajili ya kuwapa upendeleo kutokana na uzito wa tatizo lenu."
"Okay daktari lakini iwe hivyohivyo."
Nilijiuliza iwe hivyo hivyo nini, sikutaka kuhoji nilikaa kitini kusikiliza majibu yetu.
Baada ya utulivu wa dakika moja mshauri alituita majina yetu.
"Herena."
"Abee."
"Mzee Joel."
"Naam."
"Majibu yenu majibu yake kama ifuatavyo ila kwa yoyote ambaye hatakubaliana na majibu haya bado ana nafasi ya kwenda mbele zaidi kupata ukweli. Lakini kipimo chetu ni cha uhakika na kutoa majibu ya kweli yasiyo na utata hata kidogo," mshauri alitulia kumeza mate na kupitisha jicho lake kwa kila mmoja kisha alisema:
"Ila kabla sijatoa majibu nini malengo yenu?"
"Ni kuwa mke wa pili wa mzee Joel," nilijibu.
"Kwa mfano mzee joel ameathirika na wewe mzima utayapokeaje majibu yako?"
“Nitayapokea kama yalivyo lakini sitaendelea na mwenzangu kwa vile hakuwa mkweli kwangu," nilijibu.
"Hapana Herena hapo utakuwa hujamtendelea haki mwenzako, ina maana wewe ukikutwa unao na yeye hana utachukua uamuzi gani?"
"Nitamsikiliza mwenyewe ana semaje, uamuzi wowote atakaoutoa itakuwa sawa kwa upande wangu."
"Eti mzee Joel vipi ukikutwa wewe upo sawa na mwenzako ameathirika utachukua hatua gani?"
"Kwa upande wangu kwa vile nina mapenzi ya dhati kwa mwenzangu sitamtenga nitakuwa naye bega kwa bega hadi mwisho wa maisha yake kwa muda wote kuwa karibu yake ili kumtoa mawazo potofu kuwa mwenye virusi hana rafiki au rafiki wa mwenye virusi ni mwenye virusi."
"Asante sana mzee Joel kuonyesha ukomavu kwenye janga hili ambalo wengi huwatelekeza wenzi wao. Je, kama wote umejikuta mpo salama mtafanyaje? Nitaanza ni Herena."
"Mmh mimi nitamshukuru Mungu kwa kunilinda pili nitazidisha mapenzi yangu kwa mwenzangu na tatu nitaendelea kuwa muaminifu kwake."
"Vizuri Herena, na mzee wangu?"
"Mimi nitamshukuru Mungu na kuendelea kuwa muaminifu na mwenye mapenzi ya vitendo yenye kutoka chini ya uvungu wa moyo wangu na kumtimizia vyote nilivyo muahidi."
"Nashukuru kuwasikieni ni watu mnaoonyesha mapenzi ya kweli kwa kila mtu kwa mwenzake. Mwisho vipi kama wote mjikute mmeathirika mtachukua uamuzi gani?" swali lile kidogo lilinitisha kwa kuonyesha ukweli fulani, lakini nilijikaza ili kupata ukweli.
"Mm’hu Herena naona kama upo mbali kidogo?" aliniuliza baada ya kuhama kimawazo.
"Aaah, nipo sawa," nilijibu huku nikijiweka sawa kitini.
"Ehe, utachukua uamuzi gani?"
"Kwa vile mimi nipo chini ya mtu nitamsikiliza mwenzangu ana semaje."
"Sawa, lakini nataka maoni yako mwenyewe."
"Nitaendelea kuwa karibu na mwanzangu na kuwa mshauri mwema katika kuafuata yote tulishauriwa na daktari na kufuata kila nilichoelezwa kulinda afya zetu."
"Mmh vizuri sana Herena na mzee wangu?"
"Mimi kama mimi naamini ukimwi si kifo bali ni ugonjwa unaotakiwa kufuata masharti yake ambayo humfanya mtu aishi maisha marefu bila tatizo, hivyo basi nami nitakuwa bega kwa bega na mwenzangu kuhakikisha hatuendi nje ya masharti ya kuishi kwa usalama."
"Nashukuru kwa uelewa wenu mkubwa ambao utanisaidia kuyasema majibu yangu bila hofu," alitulia kwa kuzichukua kalatasi za majibu juu ya meza na kuzipitia kwa mara ya mwisho kisha alituuliza swali:
"Mmesema mahusiano yenu yana muda gani?"
"Mmh ni mwaka wa tatu sasa," nilijibu kwa niaba ya wote.
"Na katika mahusiano yenu huwa mnatumia kinga au bila kinga?"
"Hutumia siku moja moja hasa kipindi cha hatari ya mimba zaidi ya hapo huwa hatutumii."
"Mmh....sawa," alivuta pumzi kwa ndani na kuzitoa kisha alisema kwa sauti ya chini iliyosikika.
" Majibu yenu yanaonyesha kama ifuatavyo nitaanza na Herena, majibu yako yanaonyesha damu yako ni salama."
Nilipiga magoti kwa mara nyingine na kunyanyua mikono juu kwa kusema:
"Asante Mungu."
Baada ya kushukuru nilirudi kitini kusikiliza majibu ya Anko yalikuwa yakisemaje, lakini niliamini yote yaliyokuja juu ya Anko ni uongo ili kututenganishe. Nilitulia tuli kusikiliza majibu ya Anko:
"Majibu ya pili ya Mr Joel yanaonyesha damu yake ni cha..."
Hakumalizia Anko alimkata kauli.
"Muongo mkubwa ndio maana nilikataa kupima vipimo vya uchochoroni."
Nilimshika Anko na kumkalisha kitini huku nikimuomba awe mtulivu.
"Mpenzi tatizo nini hebu tumsikilize kwanza nawe utazungumza nakuomba uwe mpole."
"Hapana Herena huyu binti anataka kunivunjia heshima yangu tu," Anko alisema huku jasho zikumtoka kwa wingi kwenye paji la uso.

Nini kitaendelea? Endelea kufuatilia Mkasa huu.
Powered by Blogger.