HADITHI: Msafara wa Mamba - 16 MWISHO

SEHEMU: MWISHO
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DR AMBE’
ILIPOISHIA:...
Baada ya kushukuru nilirudi kitini kusikiliza majibu ya Anko yalikuwa yakisemaje, lakini niliamini yote yaliyokuja juu ya Anko ni uongo ili kututenganishe. Nilitulia tuli kusikiliza majibu ya Anko:
"Majibu ya pili ya Mr Joel yanaonyesha damu yake ni cha..."
Hakumalizia Anko alimkata kauli.
"Muongo mkubwa ndio maana nilikataa kupima vipimo vya uchochoroni."
Nilimshika Anko na kumkalisha kitini huku nikimuomba awe mtulivu.
"Mpenzi tatizo nini hebu tumsikilize kwanza nawe utazungumza nakuomba uwe mpole."
"Hapana Herena huyu binti anataka kunivunjia heshima yangu tu," Anko alisema huku jasho zikumtoka kwa wingi kwenye paji la uso.
SASA ENDELEA...
Baada ya kutulia huku akitweta nilimruhusu mshauri aendelee
"Kwanza kabla ya kumalizia kutoa majibu kuna kitu nataka nikiweke wazi. Mr Joel kwa tabia yako utaendelea kuueneza ukimwi kwa kutumia pesa zako kuwahonga washauri na madaktari wasiojua thamini ya maisha ya watu.
“Hivi hiyo laki tano yako inalingana na uhai wa Herena? Kama kweli ulikuwa ukimpenda Helena kwa nini usimwambie ukweli kuwa wewe ni muathirika ili mjue mjikinge vipi kuliko kuueneza bila woga.
“ Ni kweli nina shida na hela lakini si kwa mtindo huu, nimejitolea kufanya kazi hii kwa ajili ya kuokoa maisha wa watu na si kuangamiza maisha ya watu. Kwa nini unaonekana ni mwelewa lakini si kwa vitendo zaidi ya kuzungumza mdomoni lakini moyoni una dhamira mbaya.
“Mr Joel kuwa na virusi vya ukimwi si aibu siku hizi watu wameelimika. Kujitangaza ni kujikinga na kujiingiza kwenye vishawishi vya kufanya ngono na watu wasio kujua. Hivi ni wangapi katika dunia hii wenye mawazo wa kiuuaji kwa kuusambaza ukimwi kwa watu wasio na hatia.
“Si kwa wanaume hata wanawake wengi wamekuwa na tabia hiyo wanapojijua wameathirika na wana pesa hutumia pesa zao kufanya mapenzi na vijana wadogo kwa kuwapa pesa nyingi na kufanya nao mapenzi bila kinga.
Huo si ujanja bali kuliangamiza taifa ambalo nguvu kazi yake ni vijana.
“ Hivyo nakuombeni kama tulivyo zungumza awali, bado mna nafasi ya kuendelea kuwa pamoja kwa kutumia kinga na kupunguza kukutana kila wakati ili kuupa mwili nafasi ya kujenga uwezo wa kujilinda.
“Namalizia kwa kutoa ushauri kwa wote waliojitolea kuokoa maisha ya watu juu ya janga lolote si ukimwi tu. Wajitoe kwa ajili ya kuokoa si kuangamiza, pesa utakayopewa ili upindeshe ukweli hujui ni bomu ambalo hata wewe linaweza kukulipukia.
“Hivyo basi tuwe wakweli na wawazi kwa yoyote atakayetaka kuangamiza wenzake kwa ajili ya pesa zake ili wafe wengi. Ni nani aliyekuambia ukimwi ni kifo, ukimwi ni ugonjwa kama ugonjwa wowote unaweza kufa na ugonjwa mwingine tofauti na ukimwi na mwenye ukimwi akaendelea kuwepo.
“Ndugu zangu kama majibu yanavyo onyesha mmoja yupo safi na mmoja ameathirika. Ni wazi Mr Joel uliisha pata ushauri juu ya ukimwi mara ya kwanza ulipokutwa nao. Nakuomba ufuate ushauri wa washauri ili uishi muda mrefu.
“Mwisho nakuombeni muondoke salama na kuendelea kuwa karibu na mwenzako katika kupeana moyo na kufarijiana."
"Siwezi kuendelea kuwa na muuaji mzoefu kumbe umenituma vocha ili uniue....Asante dada yangu Tanzania tukiwa na moyo kama wako ile kauli mbiu ya Rais Tanzania bila ukimwi unawezekana.
“Lakini kwa walio tanguliza masrahi yao binafsi ambayo hayainufaishi nchi kauli hiyo itakuwa sawa na kumpigia mbuzi gitaa," nilijikuta nikizungumza kwa uchungu baada ya kugundua Anko kila siku alikuwa akinizunguka na kuitafuta roho yangu kama Zilairi mtoa roho.
"Nooo sivyo hivyo dada huyu bwana hafai lazima nimfungulie kesi kwa kosa la mauaji."
"Hapana usifanye hivyo watu hawa ni kuwaelimisha tu."
"Hivi ni wangapi amewaambukiza akiwemo mama yangu mzazi hakulidhika aliitaka na roho yangu."
"Herena ni shetani lakini bado nakupenda na nina mipango mingi juu yako," Anko alinipigia magoti mbele yangu kuniomba msamaha.
"Mipango mingi ya kuniondoa duniani kwa kuwahonga wote wanajihusisha na upimaji wa maambukizi ya ukimwi."
"Samahani mzee Joel pesa yako hii hapa," yule mshauri alitoa laki tano na kumpa Anko lakini niliziwahi na kuzichukua kisha nilimrudishia yule mshauri.
"Asante yako kwa kuokoa maisha yangu."
"Hapana, nashukuru," mshauri alizikataa.
"Si kweli ulichokifanya ni ujasiri wa ajabu hii hela nakupa mimi naomba upokee."
Alipokea zile hela kisha nilimuaga na kuondoka huku Anko akinifuata kwa nyuma. Nilipofika kwenye gari langu niliingia ndani na kung'oa nanga japo aliniita na kulikimbilia gari langu.
Nilikwenda hadi nyumbani ambako nilimkuta mama na kumweleza hali halisi juu ya hali ya Anko na ujanja aliousema Mai juu ya kuhonga watoa majibu.
"Nina imani ukweli umeupata sasa unasemaje?"
"Siwezi kumtenga ila nitakuwa naye karibu kama sehemu ya familia si mpenzi na nina mpango wa kutafuta mchumba wa kweli ili anioe."
"Nina amani sasa utaamini kinywa cha mkubwa kinanuka lakini maneno yake hayanuki."
"Ni kweli mzazi wangu hili limekuwa kusudio la Mungu ili liwe fundisho kwa wengine."
"Nina imani ukijiunga na kikundi cha kutoa ushauri utakuwa mwalimu mwema."
"Mmh nitaweza?"
"Kwani hao wameweza vipi ushinde wewe unayejua ABC ya maambukizi ya ukimwi."
"Nitajaribu."
Tukiwa katikati ya mazungumzo tulishangaa kumuona Anko amesimama mbele yetu kama mwanga aliyekamatwa mchana. Nilijikuta nikipandwa na hasira na kunyanyuka kitini na kumfukuza.
"Nakuomba utoke muuaji mkubwa."
"Hapana Herena hebu msikilize anataka kusema nini," mama aliingilia kati.
"Hapana mama siwezi kumsikiliza kwa lolote muuaji."
"Herena nasema rudi nyuma na ukae chini, hata kama ungeambukizwa nisinge mlaumu, ni wewe uliyeanza kununua vyeti kuficha ukweli leo ndio umejua athari zake," kauli ya mama ilinifanya niwe mpole ghafla na kumuacha Anko aseme kilicho mleta:
"Ndiyo baba unasemaje?" mama alimuuliza kwa sauti ya chini.
"Leo nimekuja kuomba msamaha kwako na kwa Herena kwa kitendo nilichokitenda ambacho si cha kibinadamu. Naweza kusema umejua nimeathirika baada ya mke wangu kupima wakati wa ujauzito.
“Na wakati huo nimeisha achana na wewe, lakini kwa Herena nilimpenda niliogopa kumwambia ukweli kutokana na kumpenda sana. Ninachokuombeni mnisamehe nami nitalipa fidia pia kuanzisha kitengo cha ushauri nasaha juu ya ukimwi ikiwa pamoja kukupeleka kusoma zaidi."
Hatukuwa na muda wa kumtafuta mchawi kwa kila mmoja wetu alikuwa na makosa. Hivyo tulikubaliana kwa pamoja kushirikiana kuanzisha NGOS kwa ajili ya kutoa matangazo juu ya kujikinga na maambukizi ya ukimwi.
****
Baada ya muda nilikwenda kusomea mambo ya ushauri nikiwa kama mkurugenzi wa shirika la NI KWELI, likiwa na maana Ni kweli ukimwi upo tuache ubishi.
Baada ya kumaliza tuliaji watu wengi, tulianza na mashule hasa kwa kutoa elimu kwa walimu kwa tabia zao chafu za kutembea na wanafunzi. Kisha tulimalizia kwa wanafunzi kwa kuelewa nini kilicho wapeleka pale shuleni ni elimu na si mapenzi.
Pia shirika letu liliandaa kongamano kubwa la vituo vyote vya ushauri nasaha na kupima virusi kwa kuwa wakweli ili kuokoa nafsi za watu. Nilitumia matukio yangu kama somo kwa wote ili tuwe wakweli na wawazi kwa kuweka masrahi ya taifa mbele kuliko kuwema maslahi binafsi.
Shirika letu kwa muda mfupi liliweka kupata misaada mingi kutoka kwa wahisani na kuweza kupanuka na kuzunguka Tanzania nzima kwa kutoa elimu ya ukimwi kwa mafanikio makubwa. Mfano wangu ndio nilioutumia kwa kutoa elimu ya kweli.
Tuligawa vipeperushi na vitabu bure mashuleni juu ya umuhimu wa elimu na kujilinda na ukimwi. Anko na mkewe walikuwa walezi ambao waliongeza nguvu kwenye kampuni yetu.
Namalizia kwa kusema Ukimwi upo na unaua, kila mmoja asimpime mwenzie kwa macho bali mkapime wote ili kujua afya zenu. Vile vile usichukulia kipimo cha mwenzako kujua afya yako bali kupewa mwenyewe.
Pia kwa wote ulijitolea kuokoa maisha ya Watanzania ili tuendane ya kauli mbinu ya mkuu wa nchi Tanzania bila ukimwi inawezekana. Kama kutanguliza maslahi ya taifa mbele na si masilahi binafsi itawezeakana.
Mwisho ni maofisini na mashuleni tusipo kuwa makini ukimwi utatumaliza hasa wanaopenda rushwa ngono ambao ndio hatari mkubwa katika kueneza virusi vya ukimwi. Namazia kwa kufuata yote tuliyozungumza tokea mwanzo wa mkasa huu Tanzania bila Ukimwi inawezekana.
Mwishooooo!!!
Post a Comment