HADITHI: Msafara wa Mamba - 14

MTUNZI: Ally Mbetu ‘DR AMBE’
ILIPOISHIA:
"Karibu mdogo wangu."
"Asante dada yangu."
"Kama sikosei ni jana tu ulikuwa hapa?"
"Ni kweli dada yangu."
"Mm’hu ulikuwa na tatizo gani?"
"Nilikuwa na swali moja juu ya maambukizi ya ukimwi."
"Uliza tu."
"Hivi kuna uwezekano mtu mwenye ukimwi kutembea na mtu asiye na ukimwi na asipate?"
SASA ENDELEA…
"Ndiyo."
"Kwa nini?"
"Inategemeana na damu ambayo uliyonayo ambayo hairuhusu virusi kuingia mwilini."
"Mmh! Ina maana mtu kama huyo kama ni mwanamke anaweza kuwa na mwanaume mwenye virusi na kuweza kuzaa nae?"
"Si vizuri kiafya hasa unapomgundua mwenzio ameathirika ni muhimu kutumia kinga muda wote."
"Kwa nini wakati siwezi kuupata huo ukimwi?"
"Sikiliza mdogo wangu mwenzio anapokuwa ameathirika na wewe kuwa salama unatakiwa kuishi naye kwa taadhari kubwa hasa katika jambo la kukutana kimwili. Huwezi kujua nguvu ya chembe zako hai zinaweza kukosa nguvu kama kila siku utazipiganisha na maradhi.
“Hivyo inaweza kuwa rahisi hata magonjwa mengine kukuingia na kukusababishia mwili wako kukosa kinga na kukufanya ufe kwa urahisi."
"Na mwenye ukimwi wa muda mrefu huweza kupoteza nguvu kwa muda gani?"
"Inategemea usikivu wake kwa kufuatilia ushauri wa wataalamu, kama atakuwa mfuatiliaji wa masharti ataishi kwa muda mrefu huku afya yake ikiwa nzuri. Lakini akienda kinyume na hapo lazima mwili wake utapoteza nguvu na kufa haraka au kuandamwa na maradhi ambayo yatamtesa mpaka kifo chake."
"Mbona kuna mtu ambaye anaonekana ni muathirika wa muda mrefu lakini bado anaendelea kuishi na hali yake nzuri japo afuatilii matibabu?"
"Si kweli kama hafuatilii masharti lazima kuna mabadiliko mwilini mwake na atakapopatwa na ugonjwa wowote ni rahisi kufa. Pia wapo wanaofanya mtindo wa kubadili damu kwa wenye pesa lakini huwa hawajui kila wanapokwenda kinyume na mashriti huuchosha mwili na siku moja hufa kama mdhaha na afya zao.
“Wengi huwa hawajui mwili unapopoteza kinga hutakiwa kufuata masharti ili kuuweka salama muda wote. Usifikili kubadili damu au kula madawa makali na kwenda kinyume na masharti yake mwili huchoka na kufika kipindi hushindwa kufanya kazi na mtu kufa ghafla." "Kwa hiyo unataka kuniambia hata mtu mwenye afya asiyefuata masharti hukumu yake ni hiyo?"
"Ni kweli kabisa."
"Sasa dada yangu nilikuwa na tatizo moja lililonirudisha kwako leo, ni hivi nina rafiki wa kiume mtu mzima ambaye ana mke. Lakini kila kona wanasema kuwa ni muathirika, lakini jana tulipopima alionekana yupo salama."
"Sasa tatizo nini?"
"Bado kuna watu wamenihakikishia kuwa ni muathirika kwa ushahidi wa vyeti, sasa utanisaidia vipi?"
"Mimi nakushauri usisikilize maneno ya watu kwa vile mmepima mmeonekana wote mpo salama, subiri miezi mitatu mkapime tena ili kujua ukweli wa mambo."
"Kuna mtu amesema kuwa Anko ananunua vyeti hapo kuna ukweli gani?"
"Mmh! Hapo pagumu kidogo..sasa ni hivi kwa vile vipimo vya hapa naviamini mwite aje hapa ili tuchukue vipimo vyetu kwa mara nyingine ukweli utajulikana tu."
"Sidhani kama atakuja vituo hivi vidogo haviamini."
'Tatizo si udogo wa kituo, cha muhimu ni mitambo ya kisasa yenye kuona vizuri bila ubabaishaji."
"Mmh ngoja nimjaribu."
"Sikiliza mdogo wangu nipe hiyo simu nitampigia mimi kumwita kuwa wewe nimekuokota hapo nje akiwa ameanguka akifika tutalazimisha akibisha mweleze ukweli. Kama kweli yupo salama atakubali."
Nilimpa simu yule dada ambaye alimpigia simu ambayo Anko aliipokea na kuahidi angefika muda si mrefu. Haikuchukua muda Anko alifika na kunikuta nimekaa mbele ya meza ya mshauri, alipofika mshauri alimkaribisha.
"Karibu mzee wangu."
"Asante" alikaa kitini huku akinishangaa.
"Vipi dear kuna tatizo gani?"
"Mmh! Afadhari umekuja, dada huyu ndiye bwana yangu naomba utupime wote," nilisema huku nikimkazia macho.
"Tupime nini tena?" aliuliza kwa mshtuko.
"Afya zetu."
"Herena sasa utakuwa mchezo si jana tu tumepima sasa vipimo vya leo vya nini, labda miezi mitatu ingekuwa imefika."
"Sikiliza Sweet siku zote ili kupata ukweli wa kitu lazima upime sehemu zaidi ya tatu ili tuwe na uhakika wa afya zetu."
"Siku zote vituo vidogo kama hivi vipimo vyake si vya kweli unaweza kukajikuta upo salama kumbe umeathirika au ujikute umeathirika kumbe upo salama."
"Kwani tatizo nini kama bado huamini vipimo vya jana ruksa twende tukarudie sasa hivi."
"Sawa lakini tuanzie hapa."
"Hapa siwezi kupima kituo hiki ni chini ya hadhi yangu."
"Wanakuja hapa hata mawaziri wenye nyadhifa serikalini itakuwa wewe, nasema hivi hapa tunapima tena," nilisisitiza baada ya kuona kama anataka kukwepa.
"Siwezi kama ndicho ulichoniitia sina muda wa kuwepo hapa tutaonana baadaye."
"Mr Joel kwa taarifa yako nakujua vizuri kuwa vyeti vyote unanunua, umemuua mama yangu na mimi unataka kuniua siyo," mtoto wa kike yalinitoka.
"Ni maneno gani hayo Herena mimi nimemuuaje mama yako?"
"Unajua vizuri sasa kama hutaki kupima siwezi kukulazimisha, ninacho kuomba kuanzia leo mimi na wewe inatosha bado nayahitaji maisha."
"Lakini kwa nini umefikia huko ni jambo la kuelewana."
"Na kuelewana ni kukubali kupima tena mimi mbona najitolea iweje wewe ukatae."
"Siviamini vipimo vya hapa."
"Aaaha kumbe unavikubali vile vya kule ambavyo umewahonga madaktari ili upate kutuua vizuri."
"Hivi Herena na maneno yako machafu nikipima na kukutwa salama utaniambia nini?" Anko alizungumza huku akitetemeka.
"Nikuambie nini zaidi ya kuongeza upendo kwako."
"Basi nipo tayari kupima," Anko alisema kwa jazba.
"Hilo ndilo lililobakia mengine hayakuwa na muhimu," nilimwambia huku mshauri akiangalia marumbano yetu.
Anko alikaa huku jasho likimtoka, mshauri alimtuliza kwa kumuuliza
"Mr nani vile?"
"Joel," Anko alijibu kwa mkato.
"Samahani Mr Joel japo kupima ni hiyari ya mtu lakini suala la kujua hali za wanamahsiano si vizuri mmoja kupima na mwenzake kutopima bado mtakuwa hamjatatua tatizo. La muhimu ni wote kujua afya zenu ili mjue muishi vipi katika kutimiza malengo yenu.
“ Kutokana na maelezo ya mwenzio kusikiliza habari za pembeni kuwa wewe ni muathirika japo mwanzo aliziba macho lakini imefikia kikomo sasa kwa hiyo una unafasi nyingine ya kudhigilisha ukweli."
"Lakini daktari si jana tu tumepima wote na kukutwa tupo salama sasa nashangaa tatizo nini?"
"Sikiliza mzee Joel kuna taarifa ambazo nina imani leo zitapata ukweli kuwa wewe una urafiki na madaktari wa hospital unayotibiwa hivyo kukufichia siri zako kwa kutoa majibu ya uongo."
"Nani kasema habari hizi za uuaji?" Anko macho yalimtoka pima.
Nini kitaendelea? Endelea kufuatilia.
Post a Comment