ad

ad

Tamasha la Jokate latikisa Sekondari ya Jangwani, Dar

IMG-20151010-WA0007 IMG-20151010-WA0012Staa wa Bongo fleva, Ally Kiba na Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ wakikamua jukwaani.IMG-20151010-WA0008Kiba na madenti wakishambulia jukwaa.
IMG-20151010-WA0009 Wanafunzi wa shule mbalimbali za wasichana jijini Dar, wakifuatilia kwa makini tamasha hilo.IMG-20151010-WA0010Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ akimpandisha stejini msanii chipukizi wa bongo fleva, Rubby jukwaani hapo.
IMG-20151010-WA0013 Rubby akifanya yake jukwaani.IMG-20151010-WA0014 Mbunifu wa mavazi, Martin kadinda akitoa neno kwa wanafunzi waliojumuika na wenzao wa Sekondari ya Jangwani kwenye tamasha la Jokate.IMG-20151010-WA0015 Kadinda na Jokate wakiteta jambo.IMG-20151010-WA0016 IMG-20151010-WA0017 Mwanadada mkali wa wimbo wa Nimempata, Pamera Daffa ‘Pam D’ akitoa burudani wakati wa tamasha hilo.IMG-20151010-WA0020 Jokate akitoa neno kwa washiriki wa tamasha hilo (hawapo pichani).IMG-20151010-WA0021
Mo Music akifanya yake jukwaani wakati watamasha hilo.
MWANAMITINDO maarufu nchini na mmiliki wa kampuni ya Kidoti Foundation, Jokate Mwegelo maarufu kwa jina la Kidoti amefanya tamasha kubwa katika shule ya sekondari Jangwani, jijini Dar es Salaam, tamasha ambalo limehudhuriwa na wanafunzi kutoka shule mbalimbali za jijini Dar es Salaam ikiwemo Jangwani, Azania, Makongo na nyingine.
Lengo kuu la tamasha hilo ilikuwa ni kuhamasisha wanafunzi katika vipaji mbalimbali ambapo walipewa fursa ya kuonesha vipaji vyao kwa kufanya shoo ya kuimba, kucheza na michezo mbalimbali na kuonesha mitindo.
Wasanii waliotumbuiza kwenye tmasha hilo ni Ally Kiba, Niki wa Pili, Pamera Daffa ‘Pam D’, Mo Music na Ruby.
Mbunifu wa mavazi, Martin Kadinda alipata fursa ya kuwazawadia wanafunzi walioweza kuonesha vipaji vyao, kiasi cha Tsh. 50,000/= kila mmoja kwa niaba yaw engine.
Pesa zilizopatikana kutokana na kiingilio kwenye ntamasha hilo zitaingizwa kwenye mfuko wa Kidoti Foundation kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wasichana wanaosoma katika mazingira magumu sehemu mbalimbali nchini.
PICHA NA MAYASA MARIWATA/GPL
Powered by Blogger.