SIMBA YAMJUMUISHA KIIZA SAFARI YA MBEYA, APISHANA NA MWAMBUSI
Mshambuliaji Hamisi Kiiza ambaye alikuwa majeruhi
anaungana na Simba katika safari ya Mbeya.
Simba inafunga safari kwenda kuivaa Mbeya City katika mechi ya Ligi Kuu Bara itakayipigwa Jumatano.
Kiiza ni kati ya wachezaji 22 wa Simba watakaosadiri
hadi Mbeya kwa ajili ya mechi hiyo.
Mbeya City itakuwa ikicheza kwa mara ya kwanza bila ya
kocha wake mkuu, Juma Mwambusi.
Mwambusi amejiunga na Yanga na sasa atakuwa Kocha Msaidizi akichukua nafasi ya Charles Boniface Mkwasa ambaye sasa ni Kocha Mkuu wa Taifa Stars.

Post a Comment