ad

ad

HADITHI: REBEKA ( Zaidi ya Mwanamke) -19


SEHEMU: 19
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’


ILIPOISHIA:
Alijua akishafanikisha zoezi lile litakalo fuata ni kumsaka Rebeka na kumrudisha nyumbani alijua lazima kakimbilia kwao. Wakati akiwa njia kuelekea Kim hotel nako Kim Hotel matajiri wanne walikuwa wakijipongeza kwa kufanikisha zoezi lao.
Walikuwa wakinywa kwa furaha huku wakiongea maneno ya kejeri.
SASA ENDELEA...

" Roja Mo ni mshamba tu hawezi kushindana na sisi mji tumempokea wenyewe hata kutongoza tumemfundisha eti leo atuzidi akili?"alisema Lemba kwa kujigamba.
"Picha tulilocheza kama ulaya vile sasa kazi kwake alipe milioni mia nne au tuzitawanye kama tulivyo mwambia sisi ndio watoto wa mjini," aliongezea Muarami.
"Tena tumekosea si anajifanya ana pesa tungemwambia milion mia sita," alisema Yusuf.
Wakiwa katikati ya maongezi mlango ulifunguliwa na kuingia Roja Mo ambaye alionekana mpole kitu kilichomtia huruma kila mmoja aliyekuwamo mule ndani. Kwa sauti ya upole alisema:
“Kwa hiyo wakubwa mnataka kiasi gani?"
"Kama tulivyo andika milioni mia nne liba ya milioni mbili tuliyo fanyia kazi," alijibu Lemba aliyekuwa na glasi ya pombe mkononi.
"Mimi nina milioni mia tatu mtapokea?"
"Hata milioni tatu na nusu hatupokei," alijibu Yusuf.
"Basi pokeeni cheki hii ya milion tatu zingine nitaleta."
Roja Mo alipitisha mkono nyuma kama anataka kuchomoa cheki walishangaa kujikuta wakitazamana na mdomo wa bastora.
"Mmefanikiwa kumuondoa ndani mke wangu lakini na ninyi mnaondoka duniani sasa tunataka tuone mmeweza kutumia milion mia mbili kuvunja ndoa yangu nataka na sasa mtumie sijui ni kiasi gani kuokoa uhai wenu," Roja Mo alisema kwa sauti ya chini.
" Roja Mo umefika mbali usifanye hivyo, tulijua tunaonyeshana jeuri ya pesa tu na si kingine," alijitetea Muarami.
"Ya kunidhalilisha au sio?"
"Lakini ni wewe uliyevunja makubaliano yetu sasa nani mwenye kosa?"
"Ikifikia hatua ya mtu kuwa na mke ilitakiwa kuheshimu kwani mpango wetu ulikuwa umekwisha kwa vile mliniahidi kufanya uliyofanya nami sina budi kufanya niliyoyaahidi kwenu. Haya kila mmoja aombe dua yake ya mwisho sipendi muingie kwenye ufalme wa mbinguni bila kujiandaa."
"Usifanye hivyo Roja Mo " Kanuth alisema huku akimsogelea Roja Mo
"Kanuth tena wewe ndiye adui yangu namba moja usinyanyue mguu rudi nyuma," Kanuth alisuasua kurudi nyuma kitu kilichomzidisha hasira Roja Mo na kuongea kwa sauti ya juu.
"Nasema moja rudi..." Kanuth alikuwa bado anaomba msamaha.
"Mbili..rudi nyuma..tatu...moja..tatu..mbili..tatu mwisho."
Hakuongeza kauli nyingine zaidi ya milio miwili iliyotua kifuani kwa Kanuth na kumtupa kwa nyuma ikiwa imehalibu vibaya kifuani na kuyachukua maisha yake.
Yusuf alijua sasa kazi imeiva alipotaka kutoa bastora yake naye alikuwa amechelewa kwani risasi mbili zilitua kwenye kifua upande wa kushoto wa moyo na kumnyamazisha palepale.
Chumba kilikuwa kikinuka damu Lemba na Muarami walijikuwa wapo kwenye wakati mgumu wa kuokoa maisha yao, Lemba aliamua liwalo na liwe aliamua kumvaa Roja Mo lakini wakati akijirusha kumvaa alikutana na risasi iliyotua kichwani iliyomfanya amuangukia Roja Mo kama mzigo.
Kitendo cha Roja Mo kuanguka na mwili wa Lemba ambaye naye alikuwa tayari mgeni wa Mungu. Mwarami alipata nafasi ya kuitoa bastora yake na kuwa tayari kwa kujihami. Roja Mo baada ya kuanguka chini aliupindua mwili wa Lemba na kutaka kummalizia Muarami.
Walijikuta kila mmoja akiachia risasi zilizompata kila mmoja kifuani na kumtupa kwa nyuma na kuchukua uhai wa kila mmoja. Ndani ya chumba kulikuwa na maiti za watu watano. Mlio wa milipuko ya risasi iliwafanya polisi waliokuwa wakimfuatilia Roja Mo waingie ndani na kwenda moja kwa moja kwenye chumba cha tukio kwa taadhari kubwa.
Ndani ya chumba walijikuta wakipingwa na butwaa kwa kukuta maiti za watu watano warafiki wakubwa lilikuwa fumbo zito ambalo hakuna aliyelijua. Polisi walizichukua maiti zote na kuzipeleka hospitali ya mkoa na kuanza uchunguzi wa vifo vya marafiki watano mara moja.
****
Rebeka aliendesha gari kwa mwendo wa masaa sita bila kupumzika na kuvuka mikoa miwili dhamira yake ni kuvuka mikoa zaidi ya mitano aende kuanza maisha mapya mpakani mwa nchi.
Aliingia mkoani majira ya saa mbili usiku aliona muda ule unafaa kutafuta sehemu ya kupumzika ili kesho aendelee na safari yake.
Alitafuta hotel yenye hadhi na kupanga, baada ya kupata chumba alijimwagia maji na kumtuma mhudumu amletee chakula hakuwa ha haja ya kutembea mwili ulikuwa umechoka sana.
Akiwa amejiegemeza kwenye tendego la kitanda akila chips kuku na bia yake ya castel macho yakiwa kwenye Luninga akiangalia taarifa ya habari. Pamoja macho yalikuwa kwenye Luninga lakini alikuwa akisinzia kwa uchovu.
Habari za mauaji ya kutisha ilimshtua baada ya kusikia sehemu aliyotoka, alitulia bila kuweka kipande cha chipsi mdomoni wala kutafuna chakula kidogo kilichobakia mdomoni na kusikiliza, alimsikia mtangazaji akisema:
"Kumetokea mauaji ya kutisha ya matajiri watano waliouana kwenye chumba cha hotel ya Kim, mpaka sasa hakuna anayejua sababu ya mauaji yale ya kutisha majina ya matajiri hao ni Roja Mo,...."Rebeka hakutaka kusikiliza tena alijikuta akiangua kilio wakati huo miili ya marehamu na sura zao zilikuwa zikionyeshwa.
Rebeka alijutia tabia yake kama angetulia kwa mume wake yote yasingemkuta, lakini alikumbuka sehemu ile haifai watu wajue yeye ni nani. Aliamua kulilia moyoni japo maumivu yake yalikuwa sawa na kukipasua kifua kwa kisu butu bila ganzi.
Alilala pale mpaka siku ya pili asubuhi alfajiri alianza safari yake ya kuelekea mpakani mwa nchi. Alitumia masaa sita kufika mpakani mji uliokuwa umechangamka sana. Alitafuta hotel yenye hadhi na kupanga pale.
Ndani ya miezi miwili Rebeka alikuwa maarufu pale mpakani, alikuwa mgeni lakini mwanamke mwenye pesa na mrembo ambaye kila tajiri alimtaka. Lakini hakuwa tayari kurudia makosa kama yaliyomkuta na kumfanya atangetange.
Kwa miezi minne alinunua jumba kubwa la milion hamsini ambalo lilikuwa likimilikiwa na mzungu ni jumba ambalo ndilo lilokuwa la kifahari pale mpakani. Kama kawaida alirudia biashara zake kwa vile alikuwa mzoefu alitengeneza hela nyingi.
Jina lake lilikuwa midomoni mwa watu lakini hakutumia tena jina la Rebeka alijiita Eva. Kila mmoja alimpenda alikuwa mwanake mwenye roho nzuri mcheshi asiye na malingo tofauti wengine ambao hata nusu ya uzuri wake hawamfikii lakini wanachagua watu wa kuongea nao.
Rebeka au Eva akiwa kwenye duka lake kubwa ambalo lilikuwa lina kila kitu na kuajili wafanyakazi zaidi ya kumi na kuwalipa mshahara mzuri. Akiwa anasoma gazeti aliona habari za kifo picha haikuwa ngeni machoni mwake.
Ilikuwa ya bwana yake Kuchu maelezo yalisema kuwa Kuchu amejiua baada ya kugundua ana ugonjwa wa upungufu wa kinga mwilini (ukimwi). Habari zile zilimshtua na kujiuliza ina maana hata yeye huenda anao anaishi nao bila kujua.
Siku ya pili aliamua kwenda hospitali kupima damu majibu hayakuwa tofauti na mawazo yake kweli alikuwa ameathirika japo hakuwa na tatizo lolote mwilini. Kila aliyemuona hawezi kuamini hata akimwueleza ameathirika ataona anataka kumnyima tu.
Aliporudi nyumbani alikuwa na mawazo mengi juu ya taarifa zile japo alijiona anapendeza machoni mwa watu lakini alikuwa muathirika maiti inayotembea au marehemu mtarajiwa.
Kweli shetani hupenda pale mtu unapokuwa na matatizo Rebeka alipata wazo baya la kutokukubali kuondoka peke yake alitaka kuacha simulizi ya marehemu kaacha orodha ndefu. Kuanzia hapo Rebeka alipunguza safari za kujijenga kimaisha kazi nyingi aliwatuma watu.

Nini kitaendelea? Kuyajua yote endelea kufuatilia.
Powered by Blogger.