HADITHI: REBEKA ( Zaidi ya Mwanamke) -17

SEHEMU: 17
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
ILIPOISHIA:
Walimalizia vinywaji vyao kwa Rebeka kukibugia chote naye Kanuth alifanya vilevile. Haikuchukua Muda Rebeka alizidiwa na zile dawa alilegea kilichoendelea hakujua. Kanuth aliwaita wanzie ambao walifanya tendo la udhalilishaji huku wakimpiga picha mnato na video.
Baada ya kufanya tendo lile walimdunga sindano ya kukata sumu ya dawa na kumuacha akiwa amelala. Waliondoka wakisherehekea ushindi mzito walioupata wa kumkomoa Roja Mo pia kumdhalilisha Rebeka.
SASA ENDELEA...
****
Sindano aliyopigwa Rebeka ilimuwahisha kuamka, alipozinzuka usingizini alijishangaa kujikuta peke yake. Mwanaume aliyejitambulisha kwake kama bwana Bingo hakuwepo hilo hakulijali alinyanyuka kitandani na kutulia kwa muda mwili ukiwa mchovu.
Alijishangaa kwa kuzidiwa na pombe si kawaida yake kuzidiwa kiasi cha kulala, siku zote hunywa kwa kipimo kilekile. Kumbukumbu zake zilimjulisha hakunywa sana, alitulia ameinama kitandani akiwa ndani ya shuka.
Kichwa alikisikia kizito alijiuliza ametumia pombe gani ambayo kwake ni ngeni. Aliamua kunyanyuka baada kusubiri bila kumuona mtu. Aliangalia saa yake ndogo ya dhahabu ya mkononi na kukuta ni saa kumi na moja jioni.
Alijiona kumbe usingizi ulikuwa mzito wa masaa zaidi ya manne. Moyoni alishukuru kuwa bwana yake Roja Mo yupo safari bila hivyo dili lake linge bumburuka. Aliamua kwenda bafuni kuoga, lakini alipoteremsha mguu alihisi maumivu makali chini ya kinena kitu kilichomfanya arudi tena kitandani.
Pembeni alipotupa macho alikuta kuna mipira ya kiume kondomu kumi na mbili zilizokwisha tumika, alijikuta akiguna.
"Mmh! Inamaana huyu bwana kanitumia kwa mipira yote hii kweli kanikomoa."
Alijilazimisha kuamka kuelekea bafuni kuoga kila hatua aliyopiga maumivu yalikuwa makali lakini aliuma meno na kwenda hadi bafuni na kuoga akiwa kwenye maumivu makali sana sehemu za siri.
Alitembea kwa shida hadi kwenye kabati na kuchukua nguo zake alizivaa kwa shida na kuamua kuondoka huku mwili ukimuuma kama kidonda hadi kwenye gari lake. Lakini alishindwa kuendesha alipojalibu kukanyaga mafuta maumivu yalikuwa makali sana kitu kilichomfanya ajilaze juu ya uskani akiwa ameuma meno.
Aliteremsha kioo na kumwita kijana mmoja ambaye alikuwa nje ya teksi yake kwa shida kwa kuwa hata alipomwita mtu kwa sauti maumivu yalikuwa makali. Bahati nzuri yule kijana alimsikia na kuja.
"Vipi sister inaonekana una matatizo mbona machozi yanakutoka?"
"Samahani kaka yangu naomba msaada wako."
"Upi huo?"
"Wewe ni dereva?"
"Ndio na gari langu hili hapo."
"Nilikuwa naomba unisaidie kunitafutia dereva ambaye atanisaidia kuniendeshea gari langu mpaka kwangu."
"Kuna malipo?"
"Kiasi chochote atakachotaka."
"Haina haja mimi natosha kwani mbali?"
"Sio mbali sana ni mjini."
"Utanipa elfu kumi na tano."
"Haina wasi ingia twende," yule dereva alikabidhi gari lake kwa mtu na kuliendesha gari la Rebeka ambaye kila muda ulivyokuwa ukienda ndivyo hali yake ilivyozidi kuwa mbaya.
"Dereva naomba unipeleke moja kwa moja Ambe Hospital."
"Kwani dada unaumwa nini?"
"Sio muhimu sana kujua kama kunifikisha hospitali," Rebeka alijibu kwa shida.
Yule kijana aliendesha kwa mwendo wa kasi ili kumwaisha hospitali. Njia nzima Rebeka aliugulia.
"Mama nakufa sijui..sijui amenifanya nini..Oooh nakufa."
Yule kijana aliyekuwa na maswali mengi kichwani lakini aliogopa kumuuliza kwa kuogopa majibu ya yule mwanamke. Aliliingiza gari Ambe Hospital hata bila maelekezo alikimbia mapokezi na kuwaeleza kuna mgonjwa mahututi.
Walikuja na machela hadi kwenye gari na kumchukua mgonjwa ambaye muda ule hakuwa na kauli. Walimbeba kwenye machela hadi wodini, dereva alijikuta akiulizwa maswali asiyoyajua.
"Eti kaka mgonjwa anatatizo gani?"
"Kwa kweli mimi sijui aliniomba msaada niendeshe gari lake nimwahishe hospitali."
"Ina maana humjui?"
"Simjui."
"Ha! huyu si Rebeka mke wa tajiri Roja Mo," muuguzi mmoja alimfahamu.
"Aaaah kweli," mwingine alimfahamu.
"Mnamjua kumbe?"dereva aliuliza.
"Ndio ni mke wa tajiri Roja Mo."
"Basi mimi nilitoa msaada tu wacha niwahi nimeacha gari langu halina mtu."
Dereva alikwenda hadi kwenye gari siku zote alijua jungu kuu halikosi ukoko. Ndani ya gari alikuta pochi ya Rebeka alipofungua alikuta kuna pesa nyingi zilikuwa kama milioni mbili. Alichukua elfu ishirini na zingine alizirudisha kisha alifunga gari na ufunguo aliwapa wahudumu wa gari ili atakapopata nafuu wampe na kuondoka zake.
****
Rebeka alizinduka saa tano za usiku na kuweza kuelezea tatizo lake aliweza kupata huduma nzuri zilizomfanya apate nafuu kwa haraka. Lakini bado ilikuwa hawezi kutembea akiwa wima kwa maumivu ya chini ya kitovu.
Daktari alimhakikishia ndani ya siku mbili angalau ataweza kusimama na kutembea japo si umbali mrefu. Lakini alimhakikishia ndani ya wiki mbili atakuwa amepona kabisa.
Rebeka akiwa amejilaza kitandani macho yakiangalia juu ya dali alijiuliza maswali mengi juu ya kitendo kile cha jana kwanza hana kumbukumbu kama alikuwa na akili zake wakati wakifanya mapenzi pili yule bwana alikuwa na uwezo gani wa kutumia Kondomu 12 peke yake tatu kwa nini ameamua kumkomoa japo kampa pesa nyingi.
Akiwa katikati ya lindi la mawazo aliingia mhudumu na kumkabidhi bahasha kubwa ambayo ilionekana ndani ilikuwa na picha. Kabla ya kuipokea alimuuliza:
"Nani kakupa?"
"Ameniambia anaitwa bwana Bingo."
"Bwana Bingo! yupo wapi?"
"Baada ya kunipa hii bahasha ameondoka na gari lake."
"Amesemaje?"
"Ameniuliza jina lako na upo wodi gani kisha alinipa bahasha hii na kuondoka."
"Akusema kitu chochote?"
"Hapana."
"Haya asante," Rebeka aliipokea ile bahasha na muuguzi alitoka nje ya chumba na kumwacha Rebeka peke yake akiifungua ile bahasha.
Baada ya kuifungua ile bahasha alikutana na picha ambazo zilikuwa zikionyesha mwanzo wa kukutana na bwana Bingo baada ya kuhalibikiwa na gari. Nyingine zilionyesha akizipokea zile pesa. Moyoni alijiuliza zile picha zina maana gani aliendelea kuchomoa picha mojamoja.
Picha zingine zilionyesha aliingia benki na nyingine zilionyesha magari mawili yakiwa yameongozana la mbele la kwake la nyuma la bwana Bingo. Nyingine zilionyesha akiingia Lyasingo Hotel na nyingine zilionyesha wakiingia chumbani na yote waliofanya ya kuvua nguo na kwenda bafuni kuoga na baada ya kuoga wakimalizia kinywaji chao.
Zilizofuata alitamani ardhi ipasuke na immeze akiwa amelazwa kitandani kama alivyozaliwa na pembeni kulikuwa na wanaume wanne na bwana Bingo alikuwepo wote wakiwa watupu.
Zilizofuata zilikuwa za udhalilishaji mkubwa ambazo hazitizamiki machoni mwa watu ni kichefuchefu. Zilikuwa zikionyesha matukio ya udhalilishaji kitendo cha kinyama alichotendewa na wanaume wale wanne ambao walimuingilia kwa zamu kila mmoja zaidi ya mara tatu.
Rebeka alitamani kulia lakini atafanyaje ni tamaa zake ndizo zimemponza. Kwa mara ya kwanza woga ulimwingia na kujiuliza Roja Mo akijuasijui itakuwaje. Aliamua kuzificha ili wahudumu wasizione.
Akili yake ilichanganyikiwa na kujiuliza maswali mengi yasio na majibu juu ya kitendo alichofanyiwa na bwana Bingo na kundi lake kumbe kutoa pesa nyingi kiasi kile kilikuwa ni kwa ajili ya kumdhalilisha. Alijiuliza na zile picha walizompiga zilikuwa za nini na kwa nini wamempelekea pale hospitali.
Alijikuta kwenye majuto makuu na kumkumbuka mume wake Mabogo na kuona heri mara mia maisha aliyokuwa akiishi na Mabogo kuliko ya muda ule. Alijiuliza sura yake atauweka wapi akikuta na na wanaume wale ni sawa na kutembea uchi japo atakuwa amevaa nguo.
Aliapa akitoka hospitali atatoroka na kwenda sehemu yoyote asiyojulikana kukimbia aibu ile.
Nini kitaendelea? Kuyajua yote endelea kufuatilia.
Post a Comment