ad

ad

HADITHI: REBEKA ( Zaidi ya Mwanamke) -16




SEHEMU: 16
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’

ILIPOISHIA:
Alikiri Roja Mo kuwa alikuwa na kila sababu kutotoa basi ule si mpira wa kutoa pasi lazima ufunge mwenyewe.
Hata Rebeka alipo nyanyuka baada ya kuokota jani alikutanisha macho na Kanuth, Koleta ambaye alikuwa hana habari kama kanuth alikuwa akimwangalia alimuuliza
"Vipi kaka yangu tayari?"
"Oooh..aah..mmh, ulisema imeharibika nini?" Kanuth alibabaika.
SASA ENDELEA...
"Aaaah kaka yangu mbona nimekueleza mapema sijui gari imenizimikia ghafla."
Kanuth hakuongea kitu alifungua boneti na kuangalia ndani labda kuna kitu kimelegea au kuchomoka. Kwa bahati nzuri alikuta ni waya wa betrii imechomoka aliokota jiwe na kuurudisha ule waya kwa kuupigilia ambao ulikaa vizuri.
Alimuomba Rebeka aingie kwenye gari na kuliwasha kwa kunyonga ufunguo. Alipowasha gari lilikubali kitu kilichomfanya Rebeka kumshukuru Kanuth.
"Oooh kaka yangu Mungu akujalie sana."
"Akujalie wewe aliyekupa upendelea wa sura umbile sina wasiwasi na tabia yako."
"Asante," Rebeka alijibu kwa kuachia tabasamu pana lililouchanachana moyo wa Kanuth na kumpa wakati mgumu kutamka kilicho mpeleka pale.
"Sasa kaka yangu sijui nikupe kiasi gani cha ufundi?"
"Hapana msaada wangu kwa viumbe kama nyinyi ni thawabu kwa Mungu, moyo wangu ungefarijika zaidi kama ungekubali mualiko wangu japo wa ghafla wa chakula cha mchana."
"Nashukuru kwa mwaliko wako hata mimi ningejisikia faraja kuongozana na wewe kupata chakula cha mchana mwanaume mwenye moyo wea huruma lakini utanisamehe kwa leo."
"Usifanye hivyo Rebeka."
"Ha! unanifahamu?"
"Rebeka nani asiyekuja hapa jijini mwanamke mwenye kila aina na uzuri na mvuto."
"Itakuwa vizuri kama unanijua ni rahisi kunielewa."
"Kukuelewa kivipi?"
"Mimi ni mke wa mtu kwa hiyo maeneo mengine siruhusiwi kwenda na mtu tofauti na mume wangu."
"Hilo nalielewa au sina hadhi ya kufuatana na wewe?"
"Mimi ni mtu wa kawaida ila naheshimu ndoa yangu vile vile mume wangu ni mtu maarufu."
"Rebeka cha mtu uliwa na mtu chuma pekee huliwa na kutu."
"Mbona sikuelewi una maana gani maana nimeona kama maongezi yamepoteza muelekeo?" Rebeka alishtuka.
"Rebeka maongezi hayajapoteza mwelekeo bali kila kiumbe anautashi wa kuongea yale yausibuyo moyo wake na siku zote mtu huutetea moyo wake mbele ya mhusika japo mke wa mtu naomba penzi lako la siku moja hata kwa saa moja na kuligharamia kwa kiasi chochote ukitakacho."
"Mmh! Usinichekeshe kaka yangu mwanaume kuugusa mwili wangu nina imani itakubidi uuze shamba la mzee wako nyumba yako kama unayo na gari zote bado nina imani itakuwa haitoshi."
Kauli ile ilimshtua Kanuth na kujiuliza huenda dau la milion mia mbili halitoshi. Lakini bado hakuonyesha kuteteleka japo moyo ulikuwa yukivuja jasho, alijikaza kiume na kumuuliza:
"Sidhani kama pesa niliyonayo ndani ya gari langu japo hailingani na hadhi ya uwezo wangu, wengine hatuna matangazo lakini mambo yetu makubwa nina imani hata huyo anayekumiliki ana pesa za kujitangaza lakini hapa anafunga breki."
Kauli ule ilimfanya Rebeka amuangalie upya Kanuth kuanzia kichwani mpaka miguuni na kumthaminisha. Ni kweli alionyesha ni mtu mwenye pesa lakini siku zote aliamini bwana yake Roja Mo ndiye mwenye pesa kuliko tajiri yoyote pale mjini.
Lakini alijua siku zote wanaume ni watu wa majingambo japo katika maisha yake hayo aliyaona miaka mingi iliyopita akiwa kijijini. Lakini toka aingie mjini wanaume wote wanaomfuata huwa wamejiandaa vilivyo.
Akiwa amejitanua kama ndege tausi kwenye hifadhi moja wapo ya taifa Rebeka aliongea kwa kujidai kuangalia yule bwana ana dau gani la chapuchapu. Hesabu aliyoweka ni milioni mia moja hamsini.
"Kwa shepu hii utanipa kiasi gani?"
"Kwa kukuonyesha uwezo wangu wa kipesa mimi ndiye naitwa bwana bingo kufanya mapenzi na mimi ni sawa na kushinda bingo."
"Ooh sikusimama kusikiliza ukijinadi kama mgombea ubunge kinachotakiwa pesa hapa penzi masilahi."
"Kwa saa moja nitakupa milioni mia mbili."
"Etiii!?" Rebeka alishtuka.
"Ndiyo wala sijakosea kutamka milion mia mbili kwa saa moja moja kwa vile ni haraka lakini tukipanga siku nzima nitakupa bilioni moja."
"Unasema kweli bwana bingo?"
"Kwa jeuri yangu pesa yenyewe ipo kwenye gari nitakupa sasa hivi nenda kaisabie kwako jioni nijulishe tuonane wapi?"
"Siamini unanitania," tamaa ya pesa ilimuingia Rebeka na kutaka kuiona ile pesa siku zote aliuapia moyo wake kuwa hata ipisha pesa aliifananisha na samaki na chambo.
Kanuth alikwenda mpaka kwenye gari na kurudi na fuko lenye pesa milioni mia mbili taslimu. Alipomfikishia aliufungua ule mfuko na kuyafanya macho ya Rebeka kukutana na maburungutu ya pesa mpya mpya tu. Moyo ulimwenda mbio na kuzitamani zile pesa na kuwa tayari kufanya naye mapenzi hata ndani ya gari.
Lakini aliogopa kuwekewa kanyaboya ilibidi aombe kuzihakikisha.
"Siamini kama zote ni pesa halali!"
"Nakuomba tuondoke na wewe hadi benki yoyote unayo iamini kisha wakusaidie kuzihakiki kisha wakusaidie na kuhesabu ili ujue tupo duniani kwa ajili ya kustarehe na viumbe wazuri kama nyinyi."
"Basi tuongozane hadi NMB."
Waliongozana pamoja kwa mbali Rebeka akiwa mbele na Kanuth nyuma hadi NMB. Rebeka aliteremka na zigo lake na kuingia benki na kumwacha Kanuth mbali na kidogo na benki akimwangalia Rebeka akiingia benki.
Muda ule Kanuth alinyanyua simu na kuwajulisha wenzie ambao muda wote walikuwa wakisubili taarifa kama zile.
"Mm’hu, lete taarifa?"
"Ndege kaishaingia kwenye mtego."
"Kwa hiyo sasa hivi upo wapi?"
"Nipo benki amekwenda kuzihakiki akitoka kitaeleweka."
"Kwa hiyo sisi tunasubili tujua wapi mnapokwenda."
"Hiyo msiwe na wasi kila mmoja ajiandae na kisu kuja kujikatia uwezo wake."
Kwa mbali Kanuth alimuona Rebeka akitoka kwenye mlango wa benki na kuingia kwenye gari lake na kwenda moja kwa moja alipo kuwa amesimamisha gari lake Kanuth.
Alipofika aliachia tabasamu pana lililozidi kumuumiza Kanuth huku akisema:
"Sasa baba kazi kwako tafuta uwanja mechi ichezwe."
"Twende Biski Hotel."
"Hapana kule mume wangu anafahamika sana."
"Basi Lyasingo Hotel."
"Kama huko sawa."
Waligeuza magari yao na safari ya kwenda Lyasingo hotel ilianza kama kawaida yao waliachana kwa mbali kitu kilichofanya mtu yoyote asitilie wasiwasi. Wakati huo Kanuth alikuwa ameisha wajulisha washikaji wake wapi waliko elekea.
Waliwasiri kama walivyopanga na kupata chumba cha bei mbaya. Baada ya kuingia ndani Kanuth alijifanya ni mtu asiye na papara lakini angekuwa peke yake angemrukia kwa sababu uzalendo ulikuwa umeushinda kuchelewa kuvua nguo kulikuwa kama kukosa alichokifuata.
Alijichelewesha kuwasubiri rafiki zake, alipopata uhakika wameishafika ndipo alipokwenda naye kuoga kabla ya mpambano. Wakiwa bafuni wakioga aliingia Mwarami na kuweka dawa ya kulevya kwenye kinywaji cha Rebeka na kutoka nje.
Walipotoka kuoga Kanuth alimuomba Rebeka wamalizie kinywaji ili mpambano uanze Naye Rebeka alikuwa kama mbwa kwa chatu baada ya kuziona milioni mia mbili alikubali chochote alichoambiwa na Kanuth.
Walimalizia vinywaji vyao kwa Rebeka kukibugia chote naye Kanuth alifanya vilevile. Haikuchukua Muda Rebeka alizidiwa na zile dawa alilegea kilichoendelea hakujua. Kanuth aliwaita wanzie ambao walifanya tendo la udhalilishaji huku wakimpiga picha mnato na video.
Baada ya kufanya tendo lile walimdunga sindano ya kukata sumu ya dawa na kumuacha akiwa amelala. Waliondoka wakisherehekea ushindi mzito walioupata wa kumkomoa Roja Mo pia kumdhalilisha Rebeka.

Nini Kitaendelea? Ili kuyajua yote endelea kufuatulia
Powered by Blogger.