ad

ad

Lulu bado amtesa mama kanumba




MAMA mzazi wa aliyekuwa staa wa filamu, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa, bado anateswa na Elizabeth Michael kufuatia maandishi yake kwenye mitandao ya kijamii katika siku ambayo ilikuwa ni kumbukumbu ya kifo cha mwanaye.
Akipiga stori na gazeti hili, Flora alisema alihuzunishwa na maneno aliyoandika mpenzi huyo wa zamani wa mtoto wake kuwa hawezi tena kumlilia Kanumba, bali watu walio muhimu kwake anaowaangalia kwa sasa ambao ni mama yake mzazi na mdogo wake, hali iliyomfanya apate presha na kulazwa hospitalini zaidi ya mara tano.
“Ukweli nina uchungu na ninaumia sana, yaani imebaki stori, haiwezi kujirudia tena kama zamani, niliumizwa sana na maneno yake mitandaoni, pia usiku ule wa siku ya kifo cha Kanumba pale Serena Hoteli alifanya sherehe na kuweka picha ya Dk. Cheni na Ali Kiba akisema ni watu muhimu kwake,” alisema mama huyo.
Powered by Blogger.