MAN UTD HAITABADILI MSHAHARA WA LUIS NANI
LONDON, ENGLAND
WINGA
Luis Nani ameelezwa kuwa hataongezwa mshahara kwa ajili ya kusaini
mkataba mpya wa miaka minne, hivyo ana hiyari ya kuondoka ama kubaki
Manchester United.
Staa
huyo wa Ureno aliitwa kwenye mkutano wiki iliyopita, na akaelezwa kuwa
klabu haitabadili mshahara wake wa pauni 90,000 kwa wiki kwa ajili ya
mkataba mwingine wa miaka minne.
Kutokana
na ombi lake la kutaka kulipwa pauni 130,000 kukataliwa, sasa staa huyo
ana uchaguzi – kuondoka ama kuendelea kubaki Old Trafford, na kama
hatasaini mkataba mpya, United itaanza kutafuta mnunuzi na kumuuza
mwisho wa msimu.
Nani
mwenye miaka 26, alijiunga United kutoka Sporting Lisbon ya Ureno kwa
pauni milioni 14, Julai 2007 na mabosi wa Old Trafford hawataki kuona
akiondoka bure atakapomaliza mkataba wake msimu ujao.

Post a Comment