Love Stori: Muhanga wa mapenzi - 01
Sehemu: 01
Mtunzi: Ally Mbetu
SIMU: 0713646500
Athumani alijikuta akiwa njia panda asijue aelekee upande gani, ilikuwa ni baada ya kumsindikiza rafiki yake aliyekuwa amekuja kunitembelea. Hii yote ilitokana na kuwa mgeni maeneo yale , akiwa amekuja kwa kaka yake ambaye alikuwa amekwenda masomoni nje ya nchi na muda huo alikuwa bado hajaoa.
Hivyo kumuita kumlindia nyumba yake, japokuwa alikuwa mgeni maeneo yale lakini hakupenda aonekane si mwenyeji wa maeneo lile. Kwa kuwa vile alipitia njia ndefu wakati wa kusindikiza aliamua apitie njia ya mkato ili niwahi nyumbani.
Cha ajabu baada ya kuingia uchochoro mmoja alijikuta nimetokea mbele ya jumba moja la kifahari. Ilimchanganya kidogo asijue nielekee upande gani . Alijiuliza nirudi au atafute kichochoro apenye. Wakati akiwa katika kujishauri mara gari la kifahari Toyota VX V8 NEW Model lilisimama mbele yake baada ya muda kidogo mlango ulifunguliwa.
Ulitangulia mguu mmoja ambao olionesha raba aina ya NIKE kisha supu ya mguu ilionesha kinachotemka si kitu cha kawaida. Naam kitu kilichoteremka si cha kawaida. Alikuwa binti mmoja mweupe akiwa katulia katika vazi la shule siketi yake iliyombana na kuonesha makalio yalivyotulia si masihara. Binti alikuwa amepewa upendelea na muumba. Baada ya kuteremka alifunga mlango wa gari na gari kuondoka.
Baada ya gari kuondoka binti yule alielekea ndani ya jumba lile la kifahari, Ahumani alionelea ni vizuri amuulize njia ya kutokea barabarani. Kabla ya kuingia getini alimwita lakini hakumjali alichepua mwendo kuingia ndani. Alifikiria labda hajamsikia. Alichapulisha mwendo na kumwahi kabla hajagusa kengele ya getini. Alipomgusa tu yule msichana alimkalipia.
“We kaka umerogwa … Usinishike wewe una hadhi ya kunishika mtu kama mimi,” alimjibu huku alijifuta sehemu aliyomshika kwa kitambaa cha mkononi.
“ Samahani sister nilikuwa nataka kukuliza,“ Athumani alisema kwa upole.
“ Uniulize uliniona na nafanya kazi mapokezi?” alimjibu kwa nyodo.
“ Samahani,” Athumani alimuomba msamaha msichana aliyeonekana ana dharau sana.
“Ninyi ndio vibaka achana na mimi.”
Mabishanoyao yalisababisha askari wa getini afungue mlango na kuhoji.
“Rachel vipi ?“ Aliuliza askari.
“ Si hili libaba eti linataka kuliuliza kama sio likibaka linataka kuniibia.”
Ilibidi mlinzi aingilie kati na kumwambia Rachel aingie ndani na kuniuliza shida yangu. Alimweleza hali halisi mlinzi alimuelewa na kumuonyesha njia ya mkato.
Baada ya kuachana na yule msichana alirudi nyumbani kuendelea na shughuli zake, maneno ya yule binti hakuyatilia maanani hasa akizingatia watoto wa kubwa. Wengi wametawaliwa na dharau
RACHEL
Rachel msichana aliyeubwa akaumbika mtoto wa tajiri mmoja jijini anayetambuliwa kwa jina la John Mulisa. Pamoja na uzuri wake alikuwa ni binti anayejiona sana si nyumbani hata shuleni alichagua rafiki wa kuzungumza naye wengi walipenda kumwita mama mashauzi.
Siku moja Rachel chumbani kwake baada ya kutoka shule jicho lake lilikuwa barabarani sehemu kulikokuwepo dirisha lake. Jicho lake lilitua kwa mvulana mmoja aliyekuwa akipita katika vazi la kuvutia pia mwili wake ulijengeka kiume hasa.
Mvulana yule alikuwa mgeni machoni kwake, alijikuta akimpenda ghafla ya kutamani siku moja awe wake. Rachel alimsindikiza kwa macho hadi alipopotea machoni kwake. Alijikuta akijiuliza kijana mzuri kama yule anakaa wapi na atawezaje kumpata mtoto wa kike. Alijukuta akiuvaa ugonjwa usio na dawa ya kumeza wala kupaka.
Alijikuta akiwa katika ugonjwa wa kupenda bila ampendaye kujua. Akiwa shule alijikuta yupo katika kipindi kigumu darasani masomo yalikuwa kero kwake baada ya muda mwingi kuutumia kumuwaza mtu asiyemjua.
************
Rachel baada ya kutoka shule alikuwa chumbani kwake alibadili nguo akiwa mbele ya dressing table iliyokuwa karibu na dirisha ambalo lipo upande wa barabarani alivutiwa na kijana mmoja aliyekuwa anapiti sawa na dirisha lake ambaye alikuwa akimuona kwa mara ya pili mfururizo .
Bila kujielewa alijikuta akipenda kila kitu alichokuwa nacho yule mvulana . kuanzia mavazi yake mwendo wake, umbo lake na sura yake . Aliacha shughuli ya kubadili nguo alinyanyuka dirisha ili aliweze kumuona vyema yule kijana wa kiume.
“Ama kweli kuna vijana wa kiume walioumbwa wakaumbika hata ukipita mbele ya watu wanakuonea wivu “ alijikuta akijisemea mwenyewe.
Baada ya yule kijana kupita alimwacha Rachel katika lindi la mawazo juu ya kijana yule na kujiuliza sijui kama atamtia tena machoni . Rachal baadaya kubadili nguo na kuvaa nguo za kupendeza alisimama mbele ya kioo na kujisifia jinsi alivyo mzuri na jinsi alivyopendeza . Alijikumbatia mwenyewe huku akisema:
“ Jinsi alivyopendeza halafu nipate kijana mzuri kama niliyemwona muda ule mbona dunia nitaisanifu.“
Rachal alizivua zile nguo na kubakia na nguo ya ndani na kujitupa katika kitanda cha sita kwa sita na kujipindua kitanda kizima huku akimuwaza yule kijana ambaye ameuteka moyo wake kwa ghafla.
Nini Kitaendelea? Usikose sehemu inayofuata hapa hapa.
SHARE SIMULIZI HII KUWAFIKIA WENGI BONYEZA HAPA CHINI

Post a Comment