JAMANI DADA MARTHA LOOO!-22
www.facebook.com/2jiachieILIPOISHIA:Alipokuwa juu ya kitanda akakaa mkao wa mechi tayari akijua anatakiwa kutoka ndani ya nyumba hiyo lakini moyoni alihakikisha anatoa mapigo ambayo, Roi anaweza kuamua asitoke tena na Martha kama kulala nje ya geti alale tu.
Roi, kuona mkao wa mama Anna alichanganyikiwa. Kama paka aliyeona panya. Akaenda kitandani kwa staili ya kuruka kama golikipa wa timu maarufu ya Ulaya...puu!!
SHUKA NAYO HAPA...
Palepale alianza kuserebuka na mchezo huku mama Anna akimwangalia kwa hisia kali kama vile alikuwa akitumbuliwa jipu.
Mama Anna aliamua kujilegeza kabisa hivyo alitoa ushirikiano wa hali ya juu bila kuonesha dalili hata ya chembe kwamba kuna jambo hakubaliani na Roi...
“E...eti baby,” aliita Roi...
“Niambie baba...”
“Unaweza kuhama pale?”
“Kuhamia wapi baba angu?”
“Nitakaposema mimi?”
“Naweza ndiyo mume wangu.”
Roi kuitwa mume ndiyo kabisa, akajikuta anawewesekea uwanjani na kelele za mahaba kama vile yeye ndiye mama Anna.
***
Kule nje, Martha alitawala benchi la nje ya duka, mawazo yake yalikuwa usahihi wa mama Anna kuwepo au kutokuwepo ndani ya nyumba ya Roi...
“Ina maana kumbe niliposema nilimsikia mama Anna akimwita Roi baby nilikuwa sahihi? Lakini hawa walikutana wapi mpaka wakafahamiana?
“Kwa pale nyumbani hapana, haiwezekani. Lini kwanza? Na ilikuaje? Siku zote, Roi anakuwepo wakati ambao na mimi nipo, akitoka kurudi usiku...
“Halafu pia mbona si muda mrefu, Roi kaja kwangu! Hawa huenda wanajuana kabla ya hapa. Itakuwa hivyo, wanajuana kabla ya hapa,” aliwaza moyoni Martha akijihisi unyonge f’lani hivi.
“Lakini wewe Mangi utakuwa unamjua vizuri sana huyu kama anayeishi hapa. Hivi, ni mwadilifu kiasi gani?” Martha alimuuliza muuza duka...
“Nani, Evender?” muuza duka aliuliza naye...
“Kwani huyu kaka mwenye nyumba hii anaitwa Evender?”
“Ndiyo.”
“Mh! Siyo Roi?”
“Mh! Mi silijui jina la Roi, namjua kama Evender.”
Martha alianza kuingiwa na wasiwasi zaidi. Akahisi huenda Roi kujiita Roi alimwingiza mkenge. Na kama ni kweli halafu mpaka wameingia kwenye uhusiano hakusema ukweli wa jina lake, Martha alianza kuona kumbe alikutana na mwanaume tapeli...
“Labda ni jina la mtaani,” alisema Martha na kuomba Mungu iwe hivyo.
Mara mzee mmoja mteja aliwasili dukani hapo na kumwangalia sana usoni Martha...
“We binti kama nakufahamu,” alisema mzee huyo...
“Mimi sikufahamu.”
“We siye mdogo wake Benard?”
Ni kweli, Martha ana kaka yake anaitwa Benard. Ni machepele ile mbaya...
“Kweli Benard ni kaka yangu,” alisema Martha...
“Sasa je? Sasa Benard ni rafiki wa mtoto wangu, Mawazo. Akili zao kama sawasawa. Mimi nilikuona siku moja tu pale Kituo cha Polisi Urafiki wakati kaka yako na Mawazo walipowekwa ndani...”
“Kweli, nimekumbuka,” alisema Martha akiwa amemkumbuka mzee huyo ambaye umri ulikwenda sana...
“Haya! Mimi naishi nyumba ile ya tatu kutoka hapa. Hapa umefuata nini sasa?” aliuliza mzee huyo huku mkono wake mmoja ulioshika noti ya shilingi mia tano ukiwa umeshaingia kwenye dirisha la kuhudumiwa dukani hapo...
“Nina shida na kaka mmoja anaishi nyumba hiyo yenye geti jekundu,” alisema Martha huku macho yake yakielekea kwenye nyumba ya Roi...
“Nani, Ismaili?” aliuliza mzee huyo.
“Kwani anaitwa Ismaili?”
“Ee... ndiyo jina lake,” alisisitiza mzee huyo huku na yeye macho yake yakitua kwenye geti la nyumba hiyo.
Martha na muuza duka wote wakabaki wametumbua macho...
“Au wewe unamsema mwingine?” aliuliza Martha...
“Jamani! Kwani kwenye nyumba hiyo kunaishi watu wangapi? Si mmoja tu, kijana kijana hivi...mweupe, ana gari lina rangi ya kijiko cha chai ‘silva’.”
“Ee...” alikubali Martha...
“Ndiyo, anaitwa Ismaili. We alikwambia anaitwaje?”
“Mimi namjua kwa jina la Roi...”
“Mh! Roi tangu lini? Yule anaitwa Ismail Twalib Mussa.”
“Mimi namjua kwa jina la Evander,” alidakia kijana muuza duka.
“Hakuna bwana. Anaitwa Ismail.”
Mara, gari jeusi lilifika na kupaki getini kwa Roi, wakashuka wanaume wawili, wakiwa wamevaa suti nyeusi. Wakatembea kuelekea pale dukani. Wakasalimia wote kisha mmoja wao akauliza...
“Jamani tuna shida na Edo...anaishi kwenye nyumba hii,” alisema akionesha kidole nyumba ya Roi...
“Sisi hatujamwona...kwenye simu vipi?” alidakia mzee huyo...
“Simu yake inaita tu hapokei,” alisema mmoja wa wanaume hao huku wakirudi ndani ya gari na kuondoka zao...
“Sasa hawa jamaa wanasema anaitwa Edo...mimi najua anaitwa Ismaili...wewe unasema unamjua kwa jina la Roi...huyu muuza duka anasema anaitwa Evender. Huyu kijana si kawaida,” alisema mzee huyo akionekana kushangaa, akamwangalia Martha...
“Kwani wewe binti, unamfahamu kivipi?” mzee huyo alimuuliza Martha huku akimshika mkono na kwenda naye kando...
“Mimi ni jamaa yangu babu...”
“Jamaa yako?”
“Ndiyo babu, kwani vipi?”
“Ha! Sasa mbona watu mtaani pote hapa wanajua ni kijana mwathirika.”
“Mwathirika?” aliuliza kwa sauti Martha, macho yakapoteza uwezo wa kuona, akaanguka chini.
***
Kule chumbani, sasa Roi alikuwa akikaribia ushindi wa pili na alishatangaza nia. Mama Anna alikuwa amemkaribisha kwa shangwe huku akimuuliza anataka kumhamishia sehemu gani katika Jiji la Dar es Salaam...
“Si...sinza ku...na kufaa...”
“Sawa, tena Kwaremi...Kwaremi ndiyo kwenyewe,” alisema mama Anna huku mikono yake yote ikiwa mgongoni mwa Roi akimpa joto ambapo mlio wa geti kubwa la nje kugogwa ulisikika kwa nguvu...
“Mungu wangu, atakuwa nani amejitoa ufahamu mpaka kuamua kugonga geti langu?” alijihoji Roi akiwa anatafuta namna ya kutoka kwa mama Anna.
Itaendelea siku ya Ijumaa endelea kushare simulizi hii kabla ya Ijumaa tukutumie Imbox
Post a Comment