ad

ad

WALIOPANDA DARAJA WAIKOMALIA ARSENAL, NGOMA HAINA MWENYEWE


 Leicester City iliyorejea Ligi Kuu England msimu huu, imeokomalia Arsenal na kumalizana nayo kwa sare ya mabao 1-1 leo.

Arsenal iliyokuwa ugenini ndiyo ilikuwa ya kwanza kufunga bao katika dakika ya 20 kupitia Alexia aliyepokea pasi safi ya Sanogo.

Dakika mbili tu baadaye, Leicester wakakomaa kibingwa na kusawazisha kwa bao la J Ulloa.
Baada ya hapo wenyeji hao waliendelea kukosakosa mara kibao.
Umahiri wa kipa wa Arsenal ndiyo uliiokoa mwishoni kwa kuwa ilionekana kufa kwenye kiungo na ushambulizi.









No comments

Powered by Blogger.