ad

ad

Kumbe Vikiungwa Vitamu - 07






“Manka haya ndiyo makosa mnayafanya sana wanawake wengi, kwa nini umuache aoge peke yake. Nenda kaoge naye ikiwezekana anza kumliza kilio cha raha bafuni.”
Mmh, mtoto wa kike haraka nilitelemsha nguo ya ndani na kubakia na upande wa kanga nyepesi na kumuwahi Mateja kabla hajajipaka sabuni. Nilipokaribia bafuni Mateja alikohoa kumaanisha kuna mtu.
“Mm..mm..mmh.”
Nilisukuma mlango na kumkuta amejipaka sabuni usoni, alipofumbua macho aliniona nipo mbele yake.
“Aah, kumbe wewe?”
“Ulidhani nani?”
“Nilifikiri kuna mtu kaingia kwa bahati mbaya.”
“Nilikwenda kutoa nguo ili tuje tuoge wote,” nilidanganya.
“Sasa mbona hukuniambia kama tunaoga wote uliondoka kimya kimya.”
“Nilijua nakuwahi.”
“Haya tuoge.”

Nilimsogelea na kuusugua mwili wangu kwake, joto langu lilimsisimua. Mmh, kuangalia kwenye kikosi wa miziga,mtutu wa mziga ulikuwa juu. Manshala mtoto wa kike niliupandia mtutu na kuufanyia ukaguzi kabla ya kuingia vitani. Mmh, weee acha tu hukuwepo bali shetani wako alikuwepo.

Mateja alikuwa kama mtu aliyekula mishikaki yenye chachandu ya Kihindi jinsi alivyotoa miguno. Taratibu nilishughulika na mtutu wa mzinga ambao ulionekana ulikuwa tayari kutupa makombora mazito kwa adui. Kutokana na utaalamu niliopewa na Bi Shuu na kujua kuufanyia usafi mtutu wa mziga, mara nilimuona Mateja akitetemeka na kutoa machozi laini.

“Vipi?”

“Aa..aah.”

“Pole.”

“Asante.”

Niliendelea kumpa mshike mshike kwa kugusa hapa na pale, najua unataka kujua niligusa wapi. Vuta subra tukikutana nitakueleza mwanaume anatakiwa aguswe wapi ili kumuongezea mahanjamu. Ila lazima mikono yako iwe laini sio migumu kama mpasua kokoto utamchubua mwenzio. Nilisahau kama tupo bafuni kwa kuendeleza mateso bila chuki.

Nilimsikia Mateja akisema.

“Manka si tunarudi ndani tumalize kwanza kuoga.”

“Waaawooo,” nilifurahia kimoyo moyo kwa kuamini mbwa mwenyewe kakimbilia kichaka cha nyani asubiri vibao vya mashavu.

Tulimalizia kuoga huku nikimsugua kila kona ya mwili kisha nilimfuta maji na kumfunga taulo nami nilipitia upande wa kanga na kutoka naye kurudi chumbani. Wakati nakaribia chumbani kwangu Bi Shuu alitokea nyuma ya bafu na kunifanyia ishara ya mdomo.

Niligeuka na kusimama ili nimsikilize alikuwa na jambo gani.

“Manka,” alisema huku akiachia tabadamu.

“Abee.”

“Hongera.”

“Ya nini?”

“Unajua kuifanya kazi umeiva kwelikweli mambo uliyofanya mimi mwenyewe hoi.”

“Asante Bi Shuu.”

“Basi usiniangushe yote tisa kumi huko mnakokwenda ukifanya makosa umetia nazi kwenye supu.”

“Bi Shuu wee acha nina usongo naye ile mbaya”

“Usikamie sana ukashindwa kuyanywa.”

“Nimekuelewa.” 

Niliagana na Bi Shuu na kuelekea chumbani kwangu na maswali mengi juu  ya tabia ya Bi Shuu kunipiga chapo kila nililokuwa nafanya. Mmh, niligeuka nielekee chumbani Bi Shuu tena aliniita.

“Manka usizime taa pia dirisha lako la nyuma liache wazi”

Niliingia ndani nikijiuliza mengi juu ya tabia za Bi Shuu Kunipiga chabo, nilijua mwanzo alitaka kujua uwezo wangu lakini baada ya kuona nimeweza hakukuwa na haja ya kunipiga tena chabo zaidi ya kusubiri matokeo. Lakini kwa upande mwingine niliamini ile ndiyo ilikuwa fainali yangu ya kujua nimefundika au nilibahatisha kwa wachovu.

Pamoja na kutaka kujua nipo katika kiwango gani, wasiwasi wangu mkubwa ulikuwa kutojiamini kwa asilimia zote kutokana na kujua kuna mtu ananiangalia. Bora angenivizia nisingejua kinachoendelea na mimi kufanya makamuzi ya nguvu.

Ndani nilimkuta Mateja amekaa kitandani, mtoto wa kike kwa usongo niliokuwa nao niliivuta kanga aliyokuwa amejifunga na kubakia kama kuku anayesubiri kuingizwa kwenye mafuta. Nami yangu nikaitupa pembeni na kubakia sale sale maua si unajua asiyejua kuchagua kabila lake Mzigua. Jamani maneno mengine sijui ni kweli au wimbo ina maana Wazigua ndiyo wasiojua kuchagua?

Tuachane na hayo wanajua waliosema si mimi, baada ya kuwa sale sale kama kuku wanaosubiri kuingizwa kwenye kalai la mafuta ya moto. Kupitia mafunzo ya Bi Shuu mwanamke kabla ya kusafiri katika bahari ya huba unatakiwa kukiandaa chombo. Sehemu hii naomba twende pamoja huonekana wanawake wengi tunakosea.

Kosa kubwa kwa wanawake wengi wakiishafika kitandani husubiri kuandaliwa wao kisha wapande kwenye chombo kuanza safari ya huba wakati mwenzake naye alihitaji kusisimliwa kama yeye. Au wengine ambao huwa kama mimi Manka kabla ya kuingia unyagoni kwa Bi Shuu kujua kabla ya safari vitu gani vinatakiwa kufanywa.

Wengi wetu hutangulia kitandani na kutega kama kicheche anavyotega kuku, akiingiza kichwa tu anatimua naye mbio kichakani. Lazima sehemu hii uitumie kuandaana kila mmoja tui likikolea nazi ruksa kutia mchele, tuko pamoja nataka nilichokipata kwa Bi Shuu nawe upande japo kiduchu.

Basi mtoto wa kike nilikiwa nimepandwa na maruhani ya mapenzi  nilikuwa kama chatu aliyeshiba na kujivuta kushida huku pumzi zikinitoka kwa shida. Nilitambaza mikono yangu laini toka kona moja kwenda nyingine hasa sehemu muhimu zenye kupandisha mahanjamu.

Nilianza kumsikia Mateja akisisimka na kuninyonga taratibu kama nyoka anavyopata shida ya kutambaa kwenye sakafu. Nilizipapasa sehemu ambazo humfanya mwanaume asisimke na kumpandisha mzuka wa mapenzi. Kila nilipogusa sehemu nilimuona akitaka kunyanyuka kama samaki pomboo anavyojitupa kwenye maji kwa madoido.

Baada ya safari ndefu nilifika mji mkuu na kufanya kituo cha muda mrefu kwa kutumia mikono mdomo na ulimi ambao ulimfanya Mateja agugumie kama  dume la njiwa lenye wivu. Niliendelea kuwajibika mpaka alipolia bila msiba huku akiomba tuingie chomboni kuianza safari ya huba yenye utamu usiisha hamu hasa kwa wanaoufahamu shati uwe mtaalamu wa kuitumia yako kalamu  ndipo utaipata tamu na kukufanya mahamumu kila uikumbukapo tamu lazima upitate hamu ya kuutafuta utamu.

Sijui tupo pamoja au nimekuchanganya, mwa kwetu siku zote chakula maandalizi, na chakula kitamu kinahitaji maandalizi ya kina na katika mwili vile vile. Huwezi kudandiwa kama baskeri na kupigwa pedeli, wakati unachemka mwenzio kesha fika zamani kalala pembeni hoi kuendelea na safari hawezi  wakati mwenzake waduduuu wadogowadoooo ndo wamecharuka Wananyemvuanyemvua.

Hapa pia kuna somo nililopata kwa Bi Shuu usikubali kuianza safari hakikisha mwakwetu kwako nawe kumetiwa mchuzi wa kutosha sio kula mkavu utakukwama kooni. Nina imani tupo pamoja au nimekuacha njia panda, mwakwetu hakikisha mpenzi wako amekuandaa mpaka hatua ya mchuzi kukolea kwenye ubwabwa hapo ruksa chakula kiliwe. Lazima wote mtakifurahia sio kuwahi kitandani kusubiri hukumu bila kujitetea.

Baada ya Mateja mchicha kukolea nazi shetani wa ngono kumpanda alitaka kuchupa mchupo wa mkizi, lakini mtoto wa kike nilimshika kifuani na kumueleza.

“Mpenzi pangu pakavu tia mchuzi,” nilikuwa na maana bado hajaniandaa ili tufurahia safari kwa pamoja. Mateja alinielewa ndipo alipoanda kuniandaa kwa kufanya ziara ya mkono na ulimi mwilini kwangu, jamani chakula kitamu kikipata muandalizi asiye na papara. Nakiri sikuwahi kukutana na raha za mwili siku zote niliamini raha zipo chini tu kumbe mwenyezi Mungu aliumba kila kiungo mwilini na makusudio yake.

Kila nilipoguswa nilihisi raha tofauti na aliponigusa kwanza, mtoto wa kike nilimaliza maneno yote mdomoni kuomba hukumu baada ya kulia zaidi ya mara mbili bila huruma ya Mateja kuendelea kunipa mateso bila chuki. Baada ya tui kukolea nazi, kile nilichotaka kukionesha kwa Mateja kilitimia.

Mtoto wa kike tuliingia kilingeni kujua mbivu na mbichi, najua unahamu kujua kilichoendelea, samahani tukutane wiki ijayo.

Mtoto wa kike nilipoguswa tu nililegea mwili ulikuwa kama umepigwa shoti ya umeme, mchezo upoanza tu nilijiachia huku nikizitoa pumzi kwa kufuata mdundo, japo nyonga haikuwa laini sana kama wamakonde nami taratibu nilinyambulika kuhakikisha sitoki nje ya biti.  Hakukuwa na ushindani kila mtu alitaka kuonesha uwezo wake kwenye medani ya mapenzi.

Kila dakika ilivyokwenda ndivyo kila mtu alipoteza ustaarabu na kutaka kuonekana anaweza kuliko mwenzake. Kila dakika iliyokwenda ilikuwa ni maajabu saba ya dunia kwa Mateja. Nina imani kabisa mwanzo aliona kama nabahatisha kutokana na kunizoe Manka wa kulala kama gogo Manka mbishi nisiyekubali usumbufu wa kugeuzwa kama chapati.

Manka nilimpania Mateja bila kujua wito ule ulikuwa na sababu, kila alivyotaka nilifanya bila hiyana kila aliponituma nilikwenda bila kubisha kila alivyoniweka nilikaa bila tatizo. Muda wote niliwajibika bila kuchoka huku nikimmwagia sifa ambazo nina imani hakuwa kupewa toka azaliwe.

Kuna kipindi mtoto wa kike nilalamika kama mtoto aliyeny’ang’anywa ziwa na mama yake, kutokana na kuufurahia mchezo nilijikuta nikilia kama naonewa kumbe raha zilikuwa zimekonga kila kona ya mwili.

“Mateja kwa nini unanitesa...kosa langu nini?” Nililalama huku nikiwajibika.

Siku zote raha ya kurap uendane na mdindo, nilibadilika mtoto wa kike na kuongeza nijuavyo nisivyofunzwa na Bi Shuu. Jamani makubwa ukishangaa ya Musa utayaona ya firauni. Ghafla Mateja machozi yakaanza kumtoka baada ya kuvamia shamba la mihogo kwa mikono na mdomo jembe nililitoa kwenye mpini na kuchimba muhogo kwa mkono.

Kila nilivyoutafuta muhongo nilimuona mtoto wa kiume akihama upande mmoja kwenda mwingine. Mmh, sikuamini nilimuonea huruma lakini siku zote ukitaka kumtiba mgonjwa wa jipu usimuonee huruma. Mateja uzalendo uliomshinda aliamua kusema.

“Manka kwa nini ulinitenda?”

“Kivipi mpenzi?”

“Vitu hivi mbona hukunipa mwanzo?”

“Mpenzi vilikuwa havijaungwa, hata vya chukuchuku havikuiva.”

“Hapana...hapana...sikubali.”

“Hukubali nini tena mpenzi?”

“Siwezi kula nisishibe heri nisipewe.”

“Mateja leo utakula mpaka utasaza nipo kwa ajili yako.”

“Na baada ya leo?”

“Mi nipo tu.”
 TUENDELEE SIKU YA KESHOOOOOOOO

No comments

Powered by Blogger.