ad

ad

PENNY AJIPONZA KWA KUTUPIA PETE YA UCHUMBA


 Penniel Mungilwa ‘VJ Penny’.

Chereko? Habari ya mjini ni kwamba aliyekuwa laazizi wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Penniel Mungilwa ‘VJ Penny’ anadaiwa kujipoza kidonda cha kumwagana na mpenzi wake huyo baada ya kutupia pete ya uchumba kidoleni.


Penniel Mwingilwa amepost kwenye Instagram picha inayoonesha mkono wake wa kushoto ukiwa juu ya usukani wa gari ambao una pete katika kidole cha chanda.

Penny ambaye ni mtangazaji wa Kipindi cha Genge cha EFM aliifanya ishu hiyo wikiendi iliyopita ambapo mwanadada huyo alitupia picha akiendesha gari huku kidoleni akiwa na pete hiyo ya uchumba iliyoambatana na maneno yaliyosomeka: “Road trip…site here we come” akimaanisha yupo njiani kuelekea saiti.
‘VJ Penny’ akiwa na Diamond kwenye picha ya pamoja.
Safu hii ilimcheki Penny ili kujua chochote juu ya pete hiyo lakini hakupatikana hewani huku akiendelea kutumiwa pongezi za kumwaga. Tusubiri! 

No comments

Powered by Blogger.