ad

ad

Barua ya wazi kwa wabunge na vyama vyote vya siasa na viongozi wote na kwa umma wa Tanzania

Na mshurukuru Mungu kwa kunipa afya na uzima mpaka leo na mpaka kufikia hapa tulipofika na kuweza kuona miaka zaidi ya hamsini ya uhuru na miaka hamsini ya Muungano  na mpaka kufikia hatuwa ya kuweza kupata katiba mpaya au mchakato wa kuandika katiba mpya,
Na wewe Bwana michuzi nashukuru kwa kazi yako unayoifanya ya kutupa matukio yanayotokea uko nyumbani kwa video na kwa picha,Mungu akurinde na akupe uzima na Afya.

Bwana michuzi wazungu wanasema  damu ni nzito kuliko maji na kubomoa ni rahishi lakini kujenga ni kazi, nayasema haya sababu Tanzania ya leo inapoelikea kuna njia ambayo ni giza na giza hilo linaweza kuleta janga ambalo lina weza umwagikaji wa damu na tukapata janga ambalo litaifanya nchi kugawanyika na  kuwa sawa sawa somalia kwa udini,ukabila,au South Sudan au nchi zingine zilozoisha pata misukosuko za west Africa liberia, Siera leon nina yasema haya kutokana na kauli zinatolewa  na baadhi ya vyama vya siasa toka vyama vya siasa vilipoanziswa,na maneno ya wabunge wa katiba.

Wa Tanzania miaka hamsini ya uhuru kuna mengi mazuri ambayo yamepatikana na mengine yalishndikana kwa sababu zetu sisi wenyewe au sera za serikari toka tulipo pata uhuru,na katika miaka hii hamsini ya muungano kuna mengi yamefanikiwa na mengine yamechukuwa muda kutatuliwa na mengine yanatakiwa kutatuliwa kwa kuangalia kule tunakotoka na kuangalia nini cha kufanya,

Dunia ya miaka ya 60 ,70,80,90,na leo kunatofauti kubwa sana kwa kifupi wakati nikiwa nasoma miaka ya 80 tulikuwa tupiga simu posta alafu posta ndio inakuunganisha na mtu wa dar au mwanza lakini leo ni sekunde, ndugu wananchi kunamambo mambo ambayo kwa ukweli lazima tuwaenzi wazee wetu hao walio tutangula Mzee Nyerere na Mzee Karume waliamua kujenga nchi mpya nchi yenye usawa nchi ambayo haina makabila nchi ambayo haina dini nchi ambayo ni ya watanzania sio wazungu wala weusi wala wahindi wala waarabu walijenga nchi ya waTanzania ambayo ina lugha moja ni kitu ambacho ni cha kujivunia nchi nying za k iAfrika zinaongea lugha za kingeni lakini Tanzania ina lugha yake ambayo siyo mkoloni.

Ndugu wananchi mimi nimeona vita ya Uganda from 83 mpaka Mzee Museveni alipochukuwa nchi 1986,vita ya Rwanda ya mwaka 1990 mpaka 1994 nimeiona na baadhi ya ndugu zangu walikufa katika hiyo vita na pia nyinyi watanzania mumeyaona na mumeyasikia ya Congo kina dada na kina mama wanavyoeteseka sana wamedakwa na kuuliwa kama wanyama sababu ya kauli za viongozi kuwa na watu wanaotaka madaraka kwa kutumia nguvu au kumwaga damu za wengine na kuwa na watu wanaojiita viongozi kumbe hawana Vision bali ni ma selfish nawaomba muwe macho na viongozi wa vyama vya siasa wawe wa CCM,CHADEMA,CUF,DP,NCCR, yule yoyote anayetumia lugha za kuleta vurugu siogopi  hapa nitasema kabisa Chadema walisema nchi haitatawalika,na juzi hapa katika bunge hili la katiba mwenyekiti wa chama cha CUF Mr lipumba aliwaita wabunge wa CCM eti ITARAHAMWE ni kitendo cha kushangaza kwa mtu aliyesoma mpaka kuwa profesa na kuamua kutumia neno kama hilo katika bunge maana yake Mr lipumba anamaanisha wana CCM wote Tanzania ni ITARAHAMWE nina omba Mr lipumba atupe jibu sababu wabunge wengi katika hilo bunge ni wana CCM

Ningependa kusema Mr Lipumba umesoma na wewe ni mwa siasa na ni kiongozi wa chama omba Radhi kwa WaTanzania kwa kutumia neno ambalo alifai katika bunge la Tanzania na kwa jamii.
Ndugu wananchi nirudi kwenye point ya katiba ni kweli tunataka katiba ya wa Tanzania na siyo ya CCM,CHADEMA,au CUF,NCCR, tunataka katiba ya Jamuhuri ya Muungano katiba yenye usawa katiba ambayo ambayo ina Raisi na makamo wake katiba ambayo ina waziri mkuu wa Tanzania bara,katiba ambayo ina waziri  waziri mkuu wa Tanzania visiwani Zanzibar katiba ambayo inaonyesha madaraka yao katiba ambayo itaongoza Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na katiba inayoonyesha ni nani amri jeshi mkuu  wa Tanzania. ndugu  maoni yangu haya ninayotowakutoka na mambo ambayo nimejifunza katika maisha au tabu namambo ambayo nimeyaona kwenye vita za wenyewe kule Uganda na kule Rwanda.

Ndugu wananchi na ndugu Wabunge, katiba si kitu kidogo na wala si kitu cha kukulupuka mumesema mengi lakini wakati umefika mumetukana lakini wakati umefika mumeitana majina lakini wakati umefika miaka ya hamsini ya uhuru imekuwa na amani na mafanikio  na miaka hamsini ya muuungano pia imekuwa na mafanikio na pia ina mengi amabayo yanatakiwa yafanyiwe marekebisho na ambayo yanatakiwa kufanywa  ninawaomba msifikiri eti kwa vile muko bungeni WaTanzania wengine hawaipendi nchi yao au watakaaa na kuendelea kusikia mambo yasiyo na maana au faida wakati nii huu mkae mutakafari kwa kirefu na muisome katiba kwa kwa kirefu kifungu kwa kifungu alafu mtuandikihe katiba ambayo italeta maendeleo kwa kizazi kinachofata,katiba ambayo ni ya wa Tanzania kama tunaenda kwenye Fedal government muundo ambao utalinda heshima ya nchi na watu wake na kuleta maendeleo.katiba ya ambayo itatujenja kiutendaji kazi katiba inayoonyesha au mwongozo wa uwajibikaji.
Cha mwisho ningependa kuwagusia Amani na maendeleo yaliyoanzishwa na Wazee wetu ndio kitu cha kujivunia kuwatukana au kuwakejeli ni kukosa adabu ni lazima kutumia majina ya kwa heshima na kuelimisha ata kama kuna makosa waliyafanya wao walikuwa ni binadamu kama wewe na mimi.
Bwana michuzi nashukuru kwa  kunipa nafasi hii tena Mungu akubariki
Mungu ibariki Tanzania na watu wake.

Mdau Yusef Israel

No comments

Powered by Blogger.