ad

ad

MTAI AMYEYUSHA MIYEYUSHO, AMPIGA KWA KO RAUNDI YA KWANZA, DAKIKA YA KWANZA, SEKUNDE YA 54



Kila mbabe ana mbabe wake, hilo ndilo limetokea usiku wa kuamkia leo kwenye Ukumbi wa PTA jijini Dar wakati bondia, Francis Miyeyusho ‘Chichi Mawe’ alipopata kkibaya.

Bondia Sukkasem Kietyongyuth wa Thailand, amempiga Miyeyusho kwa KO katika raundi ya kwanza, dakika ya kwanza sekunde ya 54.
Miyeyusho ambaye alianguka kama mzigo na kuwashangaza mashabiki wengi, alionekana kushangazwa na kasi ya Mthai huyo.
Wakati anaingia ulingoni alionyesha kujiamini, lakini baada ya dakika ya kwanza tu alikuwa ameishaanguka chini, akajitahidi akainuka.
Lakini Sukkasem akaendeleza mashambulizi mfululizo na kumuangusha tena, safari hii mwamuzi Emmanuel Mlundwa akalazimika kumaliza pambano.

CHANZO SALEHJEME.COM

No comments

Powered by Blogger.