ad

ad

Wachezaji Mtibwa Sugar wagoma

WACHEZAJI wa timu ya Mtibwa Sugar wametangaza kugomea mazoezi ya timu hiyo ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu baada ya kukaa miezi miwili bila ya kulipwa mishahara.

Kutokana na hali hiyo wachezaji hao wamesema kuwa hawatafanya mazoezi hayo na wataendelea kukaa nyumbani hadi siku ambayo uongozi wa timu hiyo utakapowalipa madai yao.

“Wote hatujalipwa mishahara ya miezi miwili, ukweli tumekubaliana kuwa hatuwezi kwenda mazoezini mpaka tutakapolipwa, kama hatupewi basi hatutakwenda,” alisema mchezaji mmoja aliyeomba asitajwe jina.
“Itabidi nilifuatilie ili nijue ukweli wake lakini hivi sasa sina chochote ninachofahamu juu ya suala hilo alisema kocha wa Mtibwa Mecky Maxime.
Powered by Blogger.